GOUT : TATIZO SUGU MIKOA YA ARUSHA,KILIMANJARO NA MANYARA,JE NYAMA YA MBUZI NDIYO CHANZO ?

Posted by Arusha by day and by night On 02:52 No comments

 Nyama ya mbuzi ikiwa imeokwa vyema tayari kwa sherehe maarufu kama ndufu
Aina mbalimbali za pombe kali zikiwa tayari kutumiwa na jamii

Nini maana ya gout.(what is gout)?

<>Gout ni moja kati ya ugonjwa wa aina ya athritis ambao husababisha maumivu makali katika viungo vya mwili kutokana na kiwango kikubwa cha uric acid kinapo
jengwa mwilini.

<>sharp uric acid crystal hujikusanya katika viungo vya mwili,maranyingi hujikusanya kwenye vidole gumba vya miguu (BIG TOE)

<>Mkusanyako wa uric acid (uitwao tophii) ambao huonekana kama uvimbe au mkusanyako wa vitu (lumps) chini ya ngozi usiokua na umbo na ukubwa

GOUT HUSABABISHWA NA NINI /
NINI CHANZO CHA GOUT
<>Gout husababishwa na vitu vingi sana ila mwanzo wake huanza kwa msongamano wa mawazo,ulevi,utumiaji wa madawa au kwa magonjwa mengine na kupelekea kupata ugonjwa huu wa gout.Hivyo kupelekea kiwango cha uric acid kwa wingi katika mwili.

<> Uric acid hutokana na kuvunjwa vunjwa kwa vitu viitwavyo PURINES. Purines hupatikana mwili mzima katika mkusanyiko wa cell ziitwazo tissue.Maranyingi uric acid huchanganyikana na damu,hupitia kwenye figo (kidney) inapotolewa mwilini ambapo hutolewa pamoja na mkojo.Lakini uric acid huweza kujengwa katika damu wakati mwili unapo ongeza kiwango cha utengenezaji wa uric acid.

<>figo linaposhindwa kutoa kiwango cha kutosha cha uric acid katika mwili iwapomtu anapo kula chakula kingi ambacho kina kiwango kikubwa cha purine Wakati kiwango cha uric acid kinapokuwa kingi katika damu,huitwa HYPERURICEMIA.Watu wengi wenye hyperuricemia haiwapelekei kupata ugonjwa wa gout.


JONGO (GOUT)

By Antipa Natural Therapies Centre,Tunduma[http://antipaherbals.co.tz/jongo.htm]

Dalili zake: Maumivu ya ghafla, hasa wakati wa usiku, makali hadi vidole vya miguu na vya mikono vinavimba, na hasa dole gumba.Hatimaye jongolinashambulia visigino, viwiko mikono, vifundo, magoti na kadhalika. Gout, wakati fulani umekuwa ukiitwa ugonjwa wa wafalme, au baridi yabisi ya matajiri, uligundulika takribani miaka 2500 iliyopita na Hippocretes. Watu wengi wakuu waliopita akiwemo John Calvin Charles Darwin, Benjamini Franklin na Martin Lutter walipata kuugua jongo hili.

Hasa hasa huathiri watu wazima wanaume, na kwa asilimia tano hadi kumi (5% - 10%) kwa wanawake. Wakati wanaume wazima ni kati ya miaka 35 hadi 50 na kuendelea, wanawake Jongo huonekana kabla ya kukoma hedhi (Menopause) wengi wenye tatizo hili, huwa pia na tatizo la mawe katika figo.

Vyanzo.
Asilimia 20 na zaidi wana upata ugonjwa huu kama urithi. Kundi lingine ni ulaji wa vyakula vyenye carbohydrates na protein kwa wingi, ulevi, kutokunywa maji ya kutosha na kutofanya mazoezi Kuna sumu Fulani katika baadhi ya vyakula maarufu kwa jina la ‘Uric Acid’. “Jongo huletwa na ongezeko kubwa la uric asid katika damu. Wakati viwango vyake vinapozi uwezo wa figo kuchuja inabidi ijikusanye katika maeneo maalumu ya viungo na kusababisha maumivu. Inaweza pia ikateka viungo vyote na kusababisha hasara kubwa ya mwili.” Natural Remedies Encyclopedia p 520 (2004) America’s master book of home remedy” Tiba zake
  • Katika wakati huu wa Jongo, swala la mlo lizingatiwe. Vyakula vyako viwe na hamirojo kwa wingi (Carbohydrates), lakini mafuta na protein vipungunzwe. Nyama iepukwe japokuwa nyama ya mbuzi inazidi ile ya wanyama wengine kwa uric acidi. Jamii za mikunde kundi la maharagwe, njegere na dengu vitumike kwa kiwango. Lengo ni kutojaza calories ili uzito usizidi na kama umezidi upunguzwe, pombe iachwe. Maji ya matunda yatumike zaidi.
  • Malimao, tumia doze ya siku kumi. Tazama maelezo katika kitabu cha ‘Karibu Ede vol 1’ sura ya “Malimao”
  • Changanya sana dawa ya unga wa miche hii mitatu: Skull cap, yarrow na valerian. Dozi; jaza kijiko cha chai kwa kikombe cha maji moto kunywa x 2 kwa siku..
  • Pia miche hii chini tengeneza kwa kipimo hicho juu na unywe vikombe 4 kwa siku. Blue violet, burdock, gentian root, mugwort, rue, birch, broom, sarsaparilla, buckthorn, ginger (tangawizi), pennyroyal, plantain, wood betony na balm of Gilead. Waweza kuchukua mche mmojawapo unaopatikana kwenu.
  • Tunda la apple, kuna tindikali iitwayo malic acid, hiyo ni nzuri sana kwa kumaliza uric acid katika damu. Hivyo tumia apple moja kila baada ya mlo mkuu wa siku au x 2 kwa siku.
  • Dawa za kuchua (liniment) za lumbago, baridi yabisi na miche yake zinafaa pia kwa Jongo zitumike; Miche kama: skullcap, pleurisy, angelica, Colombo, aloe vera valerian, getian na kadhalika.
  • Ndizi inaaminika kwa kazi nzuri ya kupunguza calories, au unene wa mwili na mafuta yake, kazi hiyo huenda pamoja na acid hii. Tumia ndizi zilizopikwa. peke yake kwa siku 4-5
  • Mkaratusi (Mlingoti :) Tengeneza juisi ya mlingoti na kuinywa. Chemsha majani mabichi kiganja cha mkono kwa lita moja ya maji chemsha dakika 3 hadi 5. AU kijiko 1 kikubwa unga katika lita 1 ya maji.
Doz: Wakubwa ni glasi 1 x2 kwa wiki 1 au kijiko 1 kikubwa katika lita 1 ya maji.


0 comments:

Post a Comment