DC-HAI AKAGUA UJENZI WA BARABARA ZA MACHAME NA MASAMA

Posted by Arusha by day and by night On 05:31 No comments

Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akizungumza na viongozi wa kata ya Machame kaskazini na wale wa Tanroads mkoani Kilimanjaro katka ofsi ya kijiji cha Nshara,Kulia kwake ni Ofisa tarafa ya Machame,Maftah Mohammed
Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akipata ufafanuzi wa Ujenzi wa Barabara ya Machame kutoka kwa Kaimu Meneja wa Tanroads mkoani Kilimanjaro,Mhandisi Reginald Massawe(Kushoto)
Mwenyekiti wa kijiji cha Nshara akimwonyesha mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga pamoja na Maofisa wa Tanroads mkoani Kilimanjaro moja ya eneo hatari kwa watumia barabara ya Machame katika kona ya Lambo
Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga na maofisa wa Tanroads wakishuhudia mifugo ikisagwa katika barabara ya Machame

Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akitoa maelekezo ya barabara ya Machame,kulia ni mmoja ya wataalamu wa ujenzi katika wilaya ya Hai,Mhandisi Peace
Mkuu wa wilaya ya Hai akiangalia moja ya eneo la barabara ya Machame ambalo lina kasoro katika ukarabati wake huku maofisa wa Tanroads mkoa wa Kilimanjaro wakitoa maelezo



 Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akipata maelezo kutoka kwa mwakilishi wa kampuni ya Mhandishi mshauri wa barabara ya Kwasadala hadi Masama,Crown Tech Consult Limited

Na Richard Mwangulube,Bomang’ombe


Mkuu wa wilaya Hai,Novatus Makunga amewaagiza viongozi wa vijijji na vitongoji vinavyopitiwa na barabara ya Machine Tools hadi Machame kuanza kutekeleza sheria ya barabara  katika kudhibiti uswagaji wa mifugo hususani ng’ombe katika barabara hiyo .


Mkuu huyo wa wilaya ametoa agizo hilo baada ya kukagua barabara hiyo ambayo ilikarabatiwa kwa kipande cha kilometa 7.9 na Wakala wa barabara nchini,Tanroads na baadaye alikagua barabara nyingine ya Kwasadala hadi Masama inayoendelea kujengwa na wakala huyo.


Akizungumza na viongozi mbalimbali wa vijiji vya kata ya Machame Kaskazini ambapo barabara hiyo imepita,aliwaeleza kuwa ni vyema  sasa wakaanza kusimamia sheria inayozuia mifugo kutembezwa barabarani badala ya wao kama viongozi kuanza kulalamika.


Viongozi hao awali walimweleza mkuu huyo wa wilaya kwamba kwa asili eneo la Machame siyo la ufugaji wa mifugo inayochungwa bali ufugaji wao ni ule wa ndani,hata hivyo limezuka wimbi la wamiliki wa Mabucha kwenda minadani na kununua ng’ombe ambao katika kuwasafirisha uamua kuwachunga barabarani na hivyo kuchangia uharibifu.


Makunga amemwagiza Kaimu meneja wa wakala wa Barabara,Tanroads mkoani Kilimanjaro Mhandisi Reginald Massawe kuandaa semina ya uelewa kwa viongozi wa vjiji na vitongoji itakayolenga kuwaelimisha sheria ya hifadhi ya barabara pamoja na mpango wa kuisimamia na kuwapa nakala ya sheria hiyo ili waanze mara moja kuitekeleza.


Amewataka viongozi hao kutoa notisi kwa wamiliki wa mabucha kuhusiana na kuanza utekelezaji wa sheria hiyo kwa lengo la kuwafahamisha kwamba kuanzia sasa watalazimika kusafirisha mifugo yao kwa njia ya barabara na ni marufuku kuswaga mifugo barabarani.


Kadhalika amewataka kushirikiana na wakala wa barabara kuwaondoa wote waliovamia maeneo ya hifadhi za barabara wakiwemo wanaondesha kilimo cha majani ya mifugo na wafanyabiashara wanaohifadhi mchanga wa ujenzi kwa kuwapa notisi kama sheria inavyotaka mapema iwezekanavyo.


Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa wilaya amemtaka Mhandisi Massawe kutuma wataalamu watakaoianisha mapungufu mbalimbali ambayo yamejitokza katika ukarabati huo wa baabara yakiwemo ya baadhi ya maeneo kutokuwa na makalvati,mikondo ya maji kutokuelekezwa kwa usahihi,baadhi ya maeneo lami kuanza kumeguka pamoja na mahitaji ya  kuweka alama za kuvuka kwa waenda kwa miguu jirani ni makanisa,misikiti na shule.


Awali mhandsi Massawe ameeleza wakala wa barabara imetumia kiasi cha shilingi milioni 1,005 kukarabati sehemu ya kilometa 7.95 ya barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 14.98.Amesema kazi zilzofanyika ni pamoja na kuondoa tabaka la lami,kuvuruga msingi wa awali,kujenga msingi mpya nakuweka tabaka jipya la lami nyepesi kwa upana wa barabara wa mita 9.0.


Amesema kuwa dosari mbalimbali zilzojitokeza ambazo walizibaini katika ziara hiyo ya mkuu wa wilaya ambazo znahtaji fedha nyingi zitafanyiwa kazi katika awamu ijayo ya kukarabati barabara hiyo ambayo itaingizwa katika mwaka ujao wa fedha ambao unaanza mwezi Julai huku ndogo ndogo wakianza kuzirekebisha mara moja.


Amesema kuwa katika mwaka ujao wa fedha kiasi cha shilingi milioni 800 zimetengwa kwa kazi ya kupanua mabega ya barabara kila upande na kujenga tabaka la lami nyepesi sehemu ya barabara yenye urefu wa kilometa 5.


Akiwa  katika barabara ya Kwasadala hadi Masama mkuu huyo wa wilaya amemtaka mkandarasi kushirikiana na viongozi wa eneo hilo katika kuhakikisha ujenzi wa makalvati ya kupitisha maji unakwenda kwa usahihi kwa lengo la kuepuesha madhara hasa nyakati za masika.


Aidha amemkatmkandarasi hiyo kutatua tatizo la baadhi ya maeneo kushindwa kupiika kutokana mvua znazonyesha sasa kwa kumwaga vifusi hasa katika maeneo yenye miteremko mikali.


Mkandarasi mpya wa barabara hiyo kampuni ya Hari Singh and Sons Limited ameahidi kurekebisha sehemu zote korofi katika kipindi hiki cha mvua wakati kazi ya ujenzi huo ambayo imefikia asilimi tano ikiwa inaendelea.


Mkandarasi huyo alianza kazi mwezi Januari mwaka huu baada ya kuvunjwa kwa mkataba wa mkandarasi wa awali katika barabara hiyo ambayo ni ahadi ya rais Jakaya Kikwete.

Utekelezaji wa mradi huo upo katika hatua za awali ambapo ujenzi wa njia yamchepuko ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa daraja la mto Namwi pamoja na ujenzi wa tabaka la kwanza la mawe yaliyosagwa unaendelea katika eneo lenye urefu wa kilometa 2


Ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa Kilometa 12.5 unatarajiwa kukamilika mwezi Januari Mwakani.


0 comments:

Post a Comment