DC HAI AIMIZA TEKNOLOJIA KATIKA KILIMO KUONDOA NJAA

Posted by Arusha by day and by night On 01:41 No comments








Na Mwandishi Wetu,Hai
Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga amesema kwamba njia pekee ya kutatua matatizo katika sekta za kilimo na mifugo ya ubora,ufungashaji na uzalishaji unaotimiza mahitaji ya soko ni kuhakikisha jitihada zinaelekezwa katika kuziba pengo la kiteknolojia katika kilimo na ufugaji

Makunga ametoa wito huo wakati alipofanya ziara ya kutembelea shamba darasa la kijiji cha Roo pamoja na kuongea na wakulima wa vikundi viwili  vya umoja na upendo vinavysimamia shamba hilo ikiwa ni sehemu ya kuanza kwa wiki ya maadhimisho ya sherehe za wakulima na wafugaji nchini yaani Nane nane.

Ameeleza kupitia mpango huo wa mashamba darasa,umeweza kuziba pengo hilo la kiteknolojia katika kilimo kutokana na idadi kbwa ya wakulima katika kijiji hicho kuanza kulima kilimo chenye tija ambacho sasa kinatoa mwelekeo wa kujikomboa kiuchumi.

Makunga ametoa mfuno wa aina ya kilimo cha migomba ambacho kinatumika sasa hivi cha migomba mifupi ambacho katika shamba moja kina uwezo wa kumpatia mkulima mikungu ya ndizi ipatayo 1350 ambapo kwa mavuno yanayochukuwa miezi kumi na mbili ana uwezo wa kutengeneza shilingi milioni 13.5 kwa kuuza kwa bei ya chini ya shilingi 10,000.

Mkuu huyo wa wilaya ameeleza kupitia mashamba hayo darasa wakulima wanapata mbegu za aina hiyo ya migomba kutokana na machipukizi kila baada ya miezi mitatu na kwenda kuotesha katika mashamba yao.

Aidha Makunga ameeleza kufarijika na kilimo cha mihogo kwa kutumia matuta kuanza kushika kasi katika eneo hilo la nyanda za kati na juu ambapo kihistoria lilikuwa halilimwi kabisa mihogo kwa kuamini kwamba ni sumu.

Ameeleza kuwa mbali na mihogo pia wananchi wa eneo hilo wanalima kwa ufanisi mkubwa viazi vitamu pamoja na majani ya kulishia mifugo hususani ng’ombe na mbuzi pamoja na kufuga aina ya kisasa ya mbuzi ambao katika soko huuzwa zaidi ya shilingi 400,000.

“Mpango huu wa uenezi wa miradi wilayani Hai yaani Spreading Hai tuliuanza mwezo Oktoba mwaka jana chini ya kaulimbiu ya Njaa na umasikini kuwa historia wilayani Hai inawezekana,hivi sasa umeonyesha mafanikio makubwa katika vijiji vya Kawaya,Roo,Mungushi na Mulama na lengo ni kuhakikisha unasambaa katika vijiji vyote ifikapo Oktoba 2014.

Katika risala yao,wakulima hao waliomba serikali kuwapatia pembejeo za kilimo kwa wakati muafaka na kumwomba mkuu huyo wa wilaya kuwa mlezi wa vikundi vyao viwili vya umoja na upendo.

0 comments:

Post a Comment