MAENDELEO YA SENSA WILAYANI HAI

Posted by MK On 07:57 No comments


WILAYA YA HAI
TAARIFA YA SENSA YA WATU NA MAKAZI, 2012
HADI TAREHE 03/09/2012

1.0 Utangulizi

Sensa ya Watu na Makazi ni utaratibu wa kukusanya, kuchambua na kusambaza takwimu za kidemografia, kiuchumi na kijamii kuhusiana na watu wote na makazi yao katika nchi kwa kipindi maalum. Kwa maana nyingine, Sensa ni zoezi maalum lenye lengo la kupata idadi ya watu wote katika nchi, kwa umri na jinsia, mahali wanapoishi, hali yao ya elimu, hali ya ajira, hali ya vizazi na vifo na hali ya makazi. 

Zoezi la  Sensa ya watu na makazi ni zoezi la Kitaifa ambapo serikali ilitoa maagizo na maelekezo kwa Wilaya zote nchini kuhusu maandalizi hadi hitimisho la zoezi hili.
Wilaya ya Hai ni miongoni mwa wilaya za serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania zilizoshiriki zoezi hili.

2.0 Maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi, 2012
2.1 Idadi ya EA

Wilaya hii ina maeneo ya kuhesabia (EAs) 430. Maeneo ya kuhesabia kwa kutumia dodoso refu yakiwa ni 145 na yakutumia dodoso fupi yakiwa ni 285.

2.2 Idadi ya wasimamizi na makarani

Katika kufanikisha zoezi hili Wilaya iliteua Wasimamizi 55, Makarani 290 wa dodoso refu, Makarani 285 wa dodoso fupi na Makarani wa akiba 14.


2.3 Mafunzo ya Sensa pamoja na vituo vya mafunzo (idadi ya walioanza, idadi ya waliohitimu na idadi ya makarani wa akiba)

Wasimamizi 55, Makarani wa dodoso refu 290 na Makarani wa akiba 14 walipatiwa mafunzo kuanzia tarehe 9 Agosti hadi 20 Agosti 2012 katika shule ya sekondari ya Hai day.Makarani wa dodoso fupi 285 walipatiwa mafunzo ya siku saba kuanzia tarehe 13 Agosti hadi 20 Agosti 2012.

Wakufunzi 15 walioteuliwa na Wilaya walitumika ipasavyo katika kuwafundisha walengwa kwa siku zote za mafunzo pia wakufunzi wa sensa ngazi ya Mkoa walifika eneo la mafunzo kuangalia maendeleo ya mafunzo na kusisitizia  baadhi ya maeneo muhimu ili kufanikisha zoezi hili ipasavyo.

2.4 Mapokezi ya vifaa (tarehe, aina ya vifaa na idadi yake)

Wilaya ilipokea vifaa  mbalimbali vya kufanyia zoezi la sensa tarehe 8 Agosti na 24 Agosti 2012 na kuvigawa kwa Wasimamizi na Makarani wa sensa kabla ya kuanza  kwa zoezi hilo. 

Orodha ya vifaa hivyo ni ifuatayo:-


NA
KIFAA
MAKISIO
VILIVYOPOKELEWA
1
SWMT 1:Dodoso la Jamii
649
800
2
SWMT 2:Dodoso Fupi
30704
30704
3
SWMT 3:Dodoso Refu
13050
12902
4
SWMT 4:Dodoso kwa ajili ya wasafiri/Waliolala Hotelini/Hospitalini
649
100
5
SWMT 5:Dodoso kwa ajili ya watu wasio na makazi maalum
649
50
6
EA Maps
430
430
7
Vitabu vya mageresho kwa Dodoso Refu
359
359
8
Vitabu vya mageresho kwa Dodoso Fupi
285
285
9
Training Manuals
8
8
10
RCC/DCC Hand book
2
1
11
Instruction manual to Junior Enumerators
285
330
12
Instruction manual to Senior Enumerators
359
359
13
Supervisors Hand book
96
96
14
Writing Boards
644
644
15
Special bags
644
644
16
Ordinary bags
644
644
17
Calender of National Events
644
644
18
Oath of Secrecy
644
644
19
Calculators
644
644
20
Boxes of Erasers
649
644
21
Boxes of Pencils 2HB
1298
564
22
Boxes of Sharpeners
649

23
Boxes of Blue biros
649
644
24
Boxes of Red biros
649

25
Marker pens- Black & Blue
80
80
26
Boxes of chalks
1941
1800
27
Note Books
644
644
28
Reflector Coats
644
0
29
Flip charts
10
0
30
Caps
644
0
31
Masking tape
40
40
32
Identity Cards
644
654
33
Stickers


34
Posters


35
Sisals Ropes

40
36
Leaflets

1000
37
Cellotapes

35
38
Empty Boxes
430
430
39
Special Cards for Passengers(NIMEHESABIWA)

200
40
Fomu za Udhibiti Ubora (Control Forms)



    - SWMT 11



    - SWMT 12A

70

    - SWMT 12B

668

    - SWMT 13A

58

    - SWMT 13B

108

    - SWMT 13C

18

    - SWMT 13D



    - SWMT 13E



    - SWMT 14

550

    - SWMT 15

1300

    - SWMT 16A

462

    - SWMT 16B

100

    - SWMT 16C

9

    - SWMT 16D



Aidha wilaya imeendelea kupokea vifaa vya nyongeza mara kwa mara ikiwa ni pamoja na madodoso marefu na mafupi,vifutio ,vichongeo na penseli kila vilipokuwa vikihitajika.

3.0 Utekelezaji wa Sensa ya Watu na Makazi, 2012

3.1 Idadi ya makarani walioanza zoezi la kuhesabu watu
Idadi ya Makarani walioanza zoezi la kuhesabu watu katika wilaya ya Hai ni
makarani 578. Makarani 293 wakiwa ni wa dodoso refu na 285 wa dodoso
fupi.

3.2 Zoezi la kutambua maeneo ya kuhesabia watu pamoja na
      changamoto za kusoma ramani
      
Zoezi la kutambua maeneo ya kuhesabia watu  lilifanywa na makarani katika   
maeneo yote ya wilaya kuanzia tarehe 22 Agosti hadi 24 Agosti 2012 na
kufanya utatuzi wa changamoto mbalimbali sehemu ambazo ramani za
maeneo husika zilionekana kutofautiana na uhalisia. 

  Changamoto zilizojitokeza wakati wa kutambua maeneo.
Wakati wa kutambua maeneo changamoto zifuatazo zilijitokeza.
 (i)Baadhi ya maeneo kutoonekana kwenye ramani. Kwa mfano kuna eneo liliachwa bila kuwekwa kwenye ramani lililopo katikati ya EA Na 04010 na 04012 Katika kijiji cha Nshara kata ya Machame Kaskazini.

Utatuzi wa changamoto hiyo.
Kwa kuwa eneo eneo lililokuwa limeachwa lina kaya nyingi ilibidi kutumia karani wa akiba wa kata hiyo kuhesabu eneo hilo.

3.3 Maeneo yaliyohesabiwa usiku wa tarehe 25/08/2012 kuamkia tarehe 26/08/2012 pamoja na changamoto zilizojitokeza.
      Maeneo yaliyohesabiwa  usiku wa tarehe 25/08/2012 ni uwanja wa ndege KIA, Hospitali za Machame,Hai na vituo vya afya,nyumba za kulala wageni na Hoteli zilizopo kata za Hai mjini,KIA,Machame kusini,Machame Kaskazini na Masama kusini.

3.4 Idadi ya EA zilizokamilika kuhesabiwa hadi kufikia tarehe 03/09/2012
 Hadi kufikia tarehe 03/09/2012 jumla ya EA 365 kati ya 430 zilikuwa
 zimekamilika kuhesabiwa,bado EA 95.

4.0       Mafanikio ya Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi, 2012
4.1 Mahusiano na viongozi wa  jamii (mfano wenyeviti wa vijiji na vitongoji)
      Hali ya mahusiano na viongozi wa jamii wakati wa zoezi la sensa ni nzuri.Viongozi hawa walitoa ushirikiano wa kutosha kwa makarani wa sensa.

4.2 Kuhesabiwa kwa hiari na kutoa ushirikiano
Idadi kubwa ya wananchi walikubali kuhesabiwa kwa hiari na walitoa    
 ushirikiano wa kutosha wakati wa zoezi hili.

4.3 Ushirikiano kutoka kwa Serikali na vyombo vya dola pale.
       Serikali na vyombo vya dola vilitoa ushirikiano mkubwa pale upinzani wa kuhesabiwa ulipojitokeza. Kwa mfano. Kuna wananchi walikataa kuhesabiwa kwa sababu za imani za dini ambapo serikali na vyombo vya dola vilishirikiana hadi wahusika wakakubali kuhesabiwa.

4.4 Makarani kufanyakazi katika hali ya amani na utulivu.
    Katika wilaya yetu makarani wote wa sensa wamefanya kazi katika hali ya   
    amani na utulivu. Hakuna tukio lolote lililoripotiwa la kuvuruga amani   
    katika maeneo ya kuhesabia.

5.0       Mapungufu/matatizo yaliyojitokeza wakati wa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi, 2012
5.1       Wakati wa mafunzo:-
(i)        kuchelewa kwa vifaa vya mafunzo. Kwa mfano wakati wa mafunzo ya Wasimamizi,Makarani wa dodoso refu na Makarani wa akiba, vitabu vya miongozo kwa watu hao vilifika siku 5 baada ya kuaza kwa mafunzo jambo lililowaweka wakufunzi katika mazingira magumu wakati wa kufundisha.

5.2       Wakati wa zoezi la kuhesabu watu:-
                    (i) Uhaba wa vifaa.
                         Wakati wa zoezi la sensa palitokea uhaba mkubwa wa vifaa hasa     
                        madodoso uliosababisha kupungua   kwa kasi ya uhesabuji na
                        kuiongezea  Wilaya gharama  kubwa za kurudufisha madodoso
                        hayo pale yalipochelewa kufika.

        (ii) Baadhi ya maeneo ya kuhesabia kuwa na idadi kubwa ya
            kaya.
                       Baadhi ya maeneo ya kuhesabia yameonekana kuwa na idadi
                       kubwa ya kaya kuliko ilivyotarajiwa jambo lililofanya kazi kuwa   
                       ngumu kwa  makarani na wasimamizi wa maeneo hayo.Kwa
                       mfano baadhi ya maeneo ya kata za Hai mjini,Machame         
                       Kaskazini,Masama kusini na Masama  Mashariki hayajakamilika
                       kuhesabiwa kutokana na wingi wa kaya.
                
                   (iii)Baadhi ya vifaa kutopatikana kabisa.
                         Baadhi ya vifaa  kama vile fulana,kofia na makoti maalum
                         (reflector  Coats havikupatikana kabisa jambo lililosababisha   
                         baadhi ya wanakaya  kutowapokea makarani wa sensa kwa      
                        kigezo kuwa makarani hao  wanaonekana tofauti na vyombo vya
                        habari vinavyotangaza karani wa sensa anavyotakiwa
                        kuonekana.

6.0             Changamoto
6.1             Wakati wa zoezi Sensa ya Watu na Makazi, 2012

      (i)  Baadhi ya wananchi kukataa kuhesabiwa.
        Baadhi ya wananchi walikataa kuhesabiwa hasa kwa kigezo cha imani za  
        dini jambo lilillosababisha kutumika kwa vyombo vya dola kama vile jeshi la
        polisi na viongozi wa ngazi mbalimbali kuwashawishi wananchi hao ili
        wahesabiwe.
                
    6.2   Mikakati iliyotumika kutatua changamoto
           (i)Viongozi wa serikali,viongozi wa dini na vyombo vya dola vilitumika
             kuwashawishi wananchi wote waliogoma hadi wakahesabiwa.
         
           (ii)Maeneo ambayo kaya zimeonekana kuwa nyingi makarani wa akiba
            Wametumika japokuwa makarani hao hawatoshelezi upungufu.
          
            (iii)Viongozi wa vitongoji na vijiji wamekuwa wakitumika kuwashawishi
            wananchi pale changamoto y akutowatambua makarani kwa kutovaa
            vazi maalum linapojitokeza.

7.0       Maoni/Mapendekezo

7.1 Kipindi kilichobaki.
Ni vema utaratibu   uliowekwa wa  kuwatumia makarani wa sensa katika zoezi la kuandikisha daftari la wakazi likatazamwa upya kwani baadhi ya makarani wanaanza kurudi vyuoni na baadhi ya shule binafsi zimeshaaza kufunguliwa.

7.2 Sensa ijayo
(i) Ngazi za Wilaya na Mikoa zinapaswa zishirikishwe ipasavyo katika maandalizi ya  zoezi la sensa kuanzia mwanzo wa maandalizi ili kupata takwimu sahihi za idadi ya   kaya na wakazi jambo ambalo litasaidia kufanya makisio sahihi ya  maeneo ya kuhesabia,vifaa,fedha,Wasimamizi na Makarani wakati wa sensa.

(ii) Muda mfupi kabla ya zoezi la sensa kuanza wataalam wa ramani wapite kwenye maeneo ya kuhesabia kwa kushirikiana na viongozi wa  Vijiji na Vitongoji ili kubaini mabadiliko yaliyotokea katika maeneo hayo na kurekebisha ramani husika.


           

0 comments:

Post a Comment