MWENGE WA UHURU WAINGIA NYUMBANI "KILIMANJARO"

Posted by MK On 08:16 No comments


Na Mwandishi Wetu,Same

Miradi 51  yenye thamani ya shilingi bilioni  5.8 itazinduliwa wakati wa mbio za mwenge mkoani Kilimanjaro.

Mwenge huo umepokelewa Leo asubuhi na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Leonidis  Gama  kutoka mkoani Manyara katika mji wa Hedaru uliopo wilayani Same mkoani Kilimanjaro

Mkuu wa mkoa Mhe Gama  amesema kati ya miradi hiyo, miradi 23 inatarajiwa kuzinduliwa   wakati wa mbio hizo  za mwenge wa uhuru huku miradi 20 itawekewa mawe ya msingi  na  miradi nane itatembelea  na wakimbiza mwenge kitaifa


Bwana Gama amefafanua kuwa  kati ya miradi hiyo 51, miradi 15 ni ya sekta ya elimu,miradi  nane ya afya, maji miradi miwili, kilimo na ufugaji miradi  sita

Aidha mkuu huyo wa mkoa  ameeleza kuwa miradi  miwili  ni ya miundo mbinu, hifadhi ya mazingira  miradi minne , biashara na ujasiriamali miradi  mitano pamoja na miradi ya utawala  na miradi mingine ya maendeleo

Mkuu huyo wa mkoa   amefafanua kuwa  serikali kuu imechangia kiasi cha shilingi   bilioni  3,607,631,886/ na mchango wa serikali za mitaa  ni shilingi   milioni  659,778250/  

Aidha nguvu za wananchi wamechangia kiasi cha shilingi 774,103,801/ na mashirika wahisani ya  kutoka mataifa mbalimbali  wamehangia kiasi cha shilingi  801,197,120/  Ameeleza Mkuu huyo wa Mkoa wa Kilimanjaro leo

Ukiwa Mkoani Kilimanjaro Mwenge wa Uhuru umeanza kwa kukimbizwa katika  Halmashauri ya Same na kesho utaendelea Mwanga ikifuatiwa na  Moshi Vijijini, Rombo,manispaa ya  Moshi, Hai na  Siha kabla ya kukabidhiwa kwa kwa Viongozi wa Mkoa wa Arusha mnamo Agosti 7, mwaka huu eneo la KIA. 

Mwenge wa Uhuru uliwashwa kwa mara ya kwanza Desemba 9 mwaka 1961,siku ya Uhuru wa Tanzania na kupandishwa katika kilele cha mlima Kilimanjaro



 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Leonidas Gama(Kulia) akipokea mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe Mbwilo
  Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Leonidas Gama(Kulia) akipokea mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe Mbwilo
 Viongozi mbalimbali wa halmashauri za wilaya na manispaa katika mkoa wa Kilimanjaro wakisubiri kupokea mwenge wa Uhuru kutoka mkoani Manyara
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Hai,Bwana Humbe(Katikati) akiwa na katibu wa CCM mkoani Kilimanjaro Bwana Kazidi(Kulia}
 Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro kutoka kulia ni Mhe Novatus Makunga(Hai),Mhe Pallangyo(Rombo),Mhe Dkt Charles Mlingwa(Siha) na Herman Kapufi wa same
 Viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Kilimanjaro kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoani Kilimanjaro Mama Nsilo Swai,Mhe Shaibu Ndemanga(DC-Mwanga),Mhe Novatus Makunga(DC-Hai) na Mhe Pallangyo ambaye ni DC-Rombo
 Mwenge eeh Mwenge Mbio mbio,mwenge tunaukimbiza mbio mbio......muda mfupi kabla ya makamanda wa mkoa wa Manyara hawajaukabidhi katika mkoa wa Kilimanjaro

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE AHUDHURIA MAZISHI YA SHEMEJI YAKE MJINI LINDI

Posted by MK On 08:55 No comments


:
Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo Julai 30,2012 amehudhuria mazishi ya shemeji yake,Marehemu Amani Kinyozi(45),aliyefariki Jumamosi iliyopita jijini Dar-es-Salaam na kuzikwa katika makaburi ya Mtandi mjini Lindi.Pichani Rais Kikwete akiweka udongo kaburini na pia akishiriki katika swala ya kumuombea marehemu mjini Lindi (Picha kwa hisani ya Ikulu)

SHULE CHACHE ZAJITOKEZA KATIKA MGOMO WILAYANI HAI

Posted by MK On 08:12 No comments

Na Richard Mwangulube,Hai

Jeshi la Polisi wilayani Hai mkoani Kilimanjaro limelazimika kumhoji katibu wa Chama cha Walimu,CWT wilayani Hai kwa tuhuma za kuwatisha na kuwatoa madarasani baadhi ya walimu wa shule za msingi na sekondari ambao wamepuuza mgomo ulioitishwa na chama hicho na kuingia madarasani na kuendelea kufundisha.

Taarifa hizo zimeeleza kuwa katibu huyo wa CWT Hai Bw Dowanson Temu alikutwa akifanya hivyo katika Shule ya Msingi Hai ambapo alifanikiwa kuwatoa madarasani walimu wote kumi na wanne huku watatu wakikataa na baadaye anadaiwa kuelekea katika shule ya sekondari ya Boma na baadaye shule ya Msingi Uhuru ambapo walimu wote wa shule hizo  walikataa kufanya mgomo na kuendelea na ufundishaji

Mkuu wa wilaya ya Hai,Mhe. Novatus Makunga amethibitisha kuhojiwa kwa katibu huyo kutokana na tuhuma za malalamiko ya walimu ambao pia wamedai kwamba walitishiwa kuletewa kundi la wenzao kwa ajili ya kuwachapa fimbo wote ambao watabainika ni wasaliti.

Ameeleza kuwa jeshi la Polisi lilianza kuwahoji maofisa wa Elimu wa halmashauri ya wilaya ya Hai na baadaye ndipo ilipofany hivyo kwa katibu Temu na baadaye kumwachia huru wakati upelelezi zaidi wa tukio hilo ukiendelea

Mkuu huyo pia alizungukia baadhi ya shule wilayani humo na kuwaakikishia walimu usalama wao kwa kuwataka waendelee na kazi wakati serikali bado ipo katika majadiliano na walimu wote nchini

Akizungumzia hali ya mgomo,Mhe Makunga ameeleza kuwa shule tatu za sekondari kati ya shule zote 44 ndizo walimu wameingia katika mgomo na amezitaja kuwa ni pamoja na Harambee na Uduru zilizoko kata ya machame kaskazini  na Kia iliyopo kata ya kia.

Kwa upande wa shule za msingi ameeleza kuwa ni shule mbili za Kibao na Mtakuja ndizo ziulizoingia katika mgomo kati ya shule zote za msingi 119

KUAPISHWA KWA WAKUU WA WILAYA WA KILIMANJARO 2012

Posted by MK On 05:43 No comments


Mkuu wa Blog,Novatus Makunga akiapishwa rasmi kuwa mkuu wa wilaya ya Hai,mnamo Mei 15,2012.

RAIS JAKAYA KIKWETE AZINDUA KARAKANA (HANGA) YA NDEGE ZA SHIRIKA LA NDEGE LA PRECISION AIR

Posted by MK On 22:59 1 comment

Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la ndege la Precision Air Bw. Michael Shirima akimkabidhi zawadi Mh Rais Dk. Jakaya Kikwete mara baada ya kuzinduz rasmi karakana na ndege za shirika hili (Hanga) kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo jijini Dar es salaam, Karakana hiyo itakuwa ikihudumia ndege za shirika hilo la mashirika mengine pia lakini pia itapokea wanafunzi walio kwenye mafunzo ya Uinjini wa ndege kutoka katika vuo vya ndani.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe pamoja na wakuu mbalimbali wa shirika la ndege la Precision Air na wafanyakazi wa shirika hilo mara baada  ya uzinduzi wa (Hanga) hiyo
Rais Jakaya Kikwete akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la ndege la Precision Air Bw. Alfonce Kioko alipokuwa akitoa maelezo  wakati wakati Rais alipokuwa akikagua  Hanga hiyo, kulia ni Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe 
Rais Jakaya Kikwete akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya shirika la ndege la Precision Air Bw. Michael Shirima katikati mara baada ya kuzindua Karakana ya ndege za shirika hilo, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la ndege la Precision Air Bw. Alfonce Kioko
Rais Jakaya Kikwete akiweka mkasi mara baada ya kukata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Karakana na ndege za shirika la ndege la Precision Air leo kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jijini Dar es salaam kulia ni Bw Bw. Michael Shirima

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya Precision Air Bw Michael Shirima wakati alipowasili katika uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere tayari kwa uziduzi wa Karakana wa ndege za  kampuni hiyo, kulia ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo Bw Alfonce Kioko, katikati ni Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe na kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadik
Mkurugenzi wa Hoteli ya Kibo Palace ya Arusha Bw Vicent Laswai naye amehudhuria katika uzinduzi huo kama mdau wa Utalii.Picha zaidi Bofya Hapa.

uchumaji chai kwa njia ya kienyeji na kisasa Tukuyu, wilayani Rungwe

Posted by MK On 22:56 No comments


Mkulima wa zao la chai akichuma chai yake kienyeji  katika mashamba ya Katumba Tukuyu mkoani Mbeya hivi karibuni

Huu ni uchumaji wa chai wa kisasa kwa kutumia chombo maalum

Kienyeji na mtoto mgongoni. Picha na Francis Godwin

MKATABA WA KUDHIBIRI BIASHARA YA SILAHA DUNIANI WAKWAMA

Posted by MK On 22:55 No comments

Ujumbe wa Tanzania  ambazo kwa mwezi mzima umeshiriki kikamilifu  hadi usiku wa manane pale ilipobidi na kuhakikisha kwamba maslahi ya Tanzania katika  majadiliano ya kidiplomasia ya nchi wanachama kuhusu  Mkataba wa Kisheria wa Kudhibiti Bishaara ya  Silaha duniani yalikuwa yamezingatiwa. 

Hata hivyo mkutano huo ulioanza Julai Mbili na kumalizika Julai 27 umeshindwa kutoa Mkataba kutokana na  wajumbe kutokukubaliana kuhusu baadhi ya vipengere ambavyo wengine walikuwa wanataka viwe sehemu ya mkataba, huku  wengine wakikataa kata kata. 

Mkataba huo kama ungepatikana  ulitarajiwa kwamba ungeleta matumaini na unafuu kwa  mamilioni ya watu ambao maisha yao kila siku yamo hatarini kutokana na  matumizi mabaya ya silaha.  Inaelezwa kwamba biashara ya silaha duniani inashika nafasi ya pili baada ya biashara ya madawa ya binadamu. 

Kutoka kushoto  mstari wa mbele ni Bw. Theobald Kazora kutoka Ofisi ya Rais, Brigedia  Jenerali Dkt. Charles  Muzanila kutoka JWTZ ambaye pia alikuwa kiongozi wa ujumbe, Kaimu Balozi, Dkt. Justin Seruhere ambaye pia alikuwa kiongozi wa ujumbe akisaidia na  Brigedia Jenerali Muzanila na  Bw. John Kinuno ambaye ni wakili kutoka Ofisi ya  Mwanasheria Mkuu wa Serikali. 

Kutoka kulia mstari wa nyuma ni Bw. Peter Macomara kutoka  Taasisi ya Kiraia, Brigedia Jenerali Venance Mabeyo kutoka  JWTZ na Kamishna Esaka Mugasa kutoka Jeshi la Polisi na Mwambata Jeshi katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa, Meja Wilbert Ibuge ambaye hayupo pichani