HAI IN DRIVE TO REVIVE COFFEE FARMING

Posted by MK On 11:16 No comments


By Arusha Times Correspondent

 Hai district will soon embark on reviving coffee farming which has drastically dropped because some farmers found it not paying back due to high  production costs and low produce prices.

The district commissioner Mr. Novatus Makunga  said coffee production in the district dropped to only 1,069.9 tonnes  during 2010/2011 compared to 2,568 in 2007/2008. Production for 2008/2009 was 2,106 tonnes but plummeted to 1,150. tonnes  in 2009/2010.

"From now on we must revive cultivation of the crop", he emphasized when he addressed the District Consultative Committee (DCC),noting that coffee has been a leading cash crop for small holder farmers in the area for many years in the past.

Another strategy to improve agriculture is through promoting irrigation farming. He said   half of the arable land totaling 46,506 hectares are suitable for irrigation but only 17,010 ha are currently under irrigation farming.

Areas which are suitable for irrigation farming include Machame Kusini, Weruweru, Masama and Rundugai wards, the DC explained, noting  that greater emphasis will be placed in areas with high potential.

On environmental conservation, the district leader decried indiscriminate felling of tress, especially on the slopes of Mt. Kilimanjaro which is the source of rivers and streams feeding  people and their livestock in the region.

To address the problem, the regional authorities have suspended issuance of permits for logging in the forest belt on the mountain and that the measure was not taken to frustrate local investors but to protect the mountain.

He added that tree felling on the slopes of the mountain has increased in recent years and that it was to blame for the decreasing rains, rising temperatures and dropping of levels of water on the streams and rivers originating there.

Although cutting of trees is rampant in villages surrounding the mountain, the situation is much worse along the banks of Kikafu river, one of the largest in the area. Most of the trees are felled for timber.

"We have directed that tree planting should be undertaken in every primary school, village and institution to take deliberate efforts to plant trees in their respective localities", he pointed out.


Copyright © 2001 -  2006  Arusha Times.  E-mail: arushatimes@habari.co.tz
Webdesigner: Grace Balende Tungaraza

DC ATOA SIKU KUMI NA NNE KWA WAVAMIZI WA VYANZO VYA MAJI VYA SHIRINJORO

Posted by MK On 20:22 No comments

 Uharibifu mkubwa wa ukataji wa kandokando ya mito katika wilaya ya Hai
Ukataji wa mito katika maeneo ya vyanzo vya maji kunakofanywa na watu waliovamia maeneo hayo

Na Richard Mwangulube,Hai

Mkuu wa wilaya ya Hai, Novatus Makunga ametoa muda wa siku kumi na nne kwa watu wote waliovamia vyanzo vya maji katika eneo la Shirinjoro wilayani Hai mkoani Kilimanjaro wawe wameondoka kwa hiari yao wenyewe.

Waandishi wa habari waliotembelea vyanzo hivyo wamekuta uzio mkubwa wa tofali ukiendelea kujengwa katika moja ya vyanzo hivi huku eneo lingine likiwa na nguzo za uzio wa waya


Mkuu huyo wa wilaya ametoa agizo hilo katika mkutano wa kijiji cha Shirinjoro aliohitisha baada ya kutembelea vyanzo vitatu vya maji na kubaini kwamba kuna uvamizi mkubwa wa shughuli za kibinadamu ndani ya maeneo hayo ambayo yanalindwa na  sheria ya mazingira.

Alisema kuwa baada ya muda huo kupita sheria itachukiwa mkondo kwa wote ambao watakaidi kwa makusudi kuondoka katika maeneo hayo ambao yanalindwa kwa mujibu wa sheria ya mazingira.


Vyanzo hivyo ni pamoja na Njoro juu,chemchemu ya Kiladeda na chanzo cha maji cha Kitifu.

Makunga ameeleza kuwa vyanzo hivyo vitatu ni muhimu kwa matumizi ya maji ya wananchi wa wilaya ya Hai pamoja na manispaa ya Moshi na kwamba vinalindwa na sheria ya mazingira na vilishatamkwa katika gazeti la serikali.


Aliwapongeza wananchi kwa kufichua uvamizi wa hivi karibuni wa wananchi wawili ambao walikuwa mbioni kuanza kujenga uzio katika vyanzo hivyo ambavyo alieleza historia inaonyesha vilianza kulindwa na viongozi wa kabla la Kichagga wanaofahamika kama Mangi.


"Ningewashanga sana endapo mngenyamazia uvamizi huu wa vyanzo vya maji ambavyo viliweza kulindwa na wazee wenu na viongozi wa wakati huo yaani Mangi,endeleeni kuvichua kila vitendo vya uharibifu wa mazingira sisi tupo saa ishirini na nne kuwatumikia,"alisema.

 
Aidha mkuu huyo wa wilaya ya Hai aliiagiza halmashauri ya wilaya ya Hai kuhakikisha inaweka mawe yanayoonyesha maeneo yasiyoruhusiwa kufanya shughuli za kibinadamu katika vyanzo hivyo vitatu pamoja na vyanzo vingine vilivyopo katika wilaya hiyo.


Kwa upande wao baadhi ya wananchi waliushtumu uongozi wa kijiji hicho kwa madai ya kuhusika na kuuza maeneo ya vyanzo hivyo vya maji hatua ambayo walilazimu kupeleka malalamiko kwa mkuu wa wilaya aliyeingilia kati na kuzuia ujenzi wa uzio kuzunguka moja ya chanzo hicho.


Hata hivyo baadhi ya wananchi waliomba kupewa muda zaidi kwa madai ya kwamba walikuwa hawafahamu kwamba hivyo ni vyanzo vya maji ambavyo vinalindwa kisheria.


Awali afisa mazingira katika halmashauri ya wilaya ya Hai,Mathew Ntilicha ameueleza mkutano huo kwamba jumla ya watu thelathini na saba wamevamia vyanzo hivyo kwa kujenga ndani ya mita thelathini kutoka pembezoni mwa vyanzo hivyo na wanapashwa kuondoka katika kipindi hicho.


Ameeleza kuwa kuanzia leo wataaanza kupita katika maeneo hayo yote kuweka alama katika nyumba zote ambazo imeingia katika eneo la vyanzo hivyo vya maji.


Ntiliacha ameeleza kuwa vyanzo hivyo vilitambuliwa rasmi kupitia gazeti la serikali mnamo mwaka 2005 na hivyo kulindwa kisheria.


RAIS KIKWETE AAGIZA KUHARAKISHWA KWA UJENZI BARABARA YA KWASADALA-MASAMA

Posted by MK On 21:56 No comments

 Rais Jakaya Kikwete akiwasili katika kijiji cha Roo kwa ajili ya uzinduzi wa barabara ya Kwasadala-Masama wilayani Hai
 Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Kilimanjaro pamoja na wilaya ya Hai pamoja na wabunge mara baada ya uzinduzi wa barabara ya Kwasadala-Masama
 Rais Jakaya Kikwete akizindua moja ya mtambo utakaotumika katika kazi ya ujenzi wa barabara hiyo
Rais Jakaya Kikwete akizindua rasmi ujenzi wa barabara ya Kwasadala-Masama(Picha zote kwa hisani ya Ikulu)


Na Mwandishi wetu,Hai

Rais Jakaya Kikwete ameagiza ujenzi wa Barabara ya Kwasadala hadi Masama,wilayani Hai mkoani Kilimanjaro uanze kwa kasi kwa kurekebishwa dosari zote zilizojitokeza.

Rais Kikwete ametoa agizo hilo katika Kijiji cha Roo kilichopo katika kata ya Masama Mashariki, wilayani humo wakati anaweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara hiyo.

Rais Kikwete alisema ujenzi wa barabara hiyo aliamua yeye ijengwe kwa sababu katika wilaya nzima ya Hai, eneo la Masama ndilo pekee ambalo halikuwa na barabara ya lami.

“Kazi imeanza, lakini kwa bahati mbaya imechelewa sana, sitaki kuingia kwenye sababu za kuchelewa na kwamba nilipoanza ziara niliarifiwa hakuna kinachoendelea,” alisema.

Alisema kuwa licha ya kudokezwa hivyo,aliamua lazima aweke jiwe la msingi na anaamini dosari zilizojitokeza zitamalizwa na ujenzi uanze kwa kasi kama ilivyotarajiwa.

Aidha Rais Kikwete aliagiza wizara ya ujenzi kuhakikisha barabara hiyo inaunganishwa kwa kiwango cha lami na barabara inayokwenda Machame kwa upande wa mashariki pamoja na Barabara ya Sanya juu inayounganisha kati ya Bomang’ombe na wilaya ya Siha kwa upande wa magharibi.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara hiyo,waziri wa Ujenzi  Dk John Magufuli aliipa Kampuni ya Atlantic Market Ltd inayojenga barabara hiyo siku 60 za kuwasilisha kwake mpango wa jinsi itakavyokamilisha ujenzi wa barabara hiyo

Dk Magufuli aliiagiza vyombo vyote vinavyowasimamia makandarasi pamoja na wahandisi ikiwemo bodi ya wakandarasi nchini (CRB) kuichukulia hatua kampuni hiyo iwapo ndani ya siku hizo 60, itakuwa haijawasilisha mpango wa kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo ya kilomita 12.5.

Waziri huyo alifafanua kwamba ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kwa gharama ya Sh5.4 bilioni ulianza Mei 2010 na ulitakiwa uwe umekamilika na kukabidhiwa mwezi Mei mwaka jana.

Dk Magufuli ameeleza kuwa mkandarasi wa kampuni hiyo ambayo mkurugenzi mkuu wake ni Gabriel Mrema aliyekuwapo wakati wa uzinduzi huo ameshalipwa Sh1.6 bilioni na ameshatengeneza certificate (vyeti) saba na zote amelipwa, kwa hiyo haidai serikali kwa kazi aliyofanya.

 ”Nina kuahidi mheshimiwa Rais mara utakapoondoka Mimi,Mkandarasi na mtaalamu mshauri tukakomeshana na kamwe sitakubali kutimuliwa kazi kwa ajili ya uzembe wake kabla mimi hujanifukuza,yeye nitakuwa nimeshamtema,”alisisitiza waziri Magufuli

Huku akishangiliwa na wananchi, Dk Magufuli alisema yeye hayupo tayari kufukuzwa kazi kwa sababu ya kilomita 12.5, hivyo anataka wahusika wawe wametangulia kufukuzwa.

Waziri Magufuli alisema baada ya Rais kuondoka eneo hilo, bodi ya wakandarasi na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (Tanroads), watakaa na mkandarasi kujua watakavyoshughulika naye.

“Nakupa siku 60 uje na mpango wa kukamilisha barabara hii, usipofanya hivyo bodi ya makandarasi ianze kukushughulikia ikiwezekana ufutwe kabisa ukandarasi ili ukavue samaki,” alisema.

Alisema haiwezekani mkataba unasainiwa, mkandarasi anafanya kazi hovyohovyo kwa kutengeneza kilomita nne za lami kwa miaka mwili, huku akihoji kama angepewa kilomita 100 ingekuwaje.

Dk Magufuli alisema huo ni mfano wa makandarasi wazalendo ambao hivi karibuni walilalamika mbele ya Rais Kikwete kuwa, wananyimwa kazi na serikali na kupendelea kampuni za nje.

Alitumia fursa hiyo kumweleza Mbunge wa Hai,Mheshimiwa Freeman Mbowe aliyekuwa ameketi jukwaa kuu kuwa, angalau sasa amefahamu mkandarasi ni tatizo katika kukamilisha barabara hiyo kwa wakati.

Aidha Dk Magufuli alimpongeza Mheshimiwa Mbowe kwa kutambua na kukiri hadharani kazi kubwa ya kuboresha huduma za kijamii inayofanywa na Rais Kikwete na kumtaka ajitahidi kuwaelimisha viongozi wenzake wa vyama vya upinzani.

“Mheshimiwa Mbowe leo umeongea maneno ya utukufu ambayo yanakubalika hata kwa mwenyezi Mungu,wewe kama kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni na mwenyekiti wa Chadema ni vyema sasa ukawaelimisha na wenzako wachache wanaojifanya hawaoni kazi zinazofanyika,”alifafanua Dk Magufuli.

Kwa upande wake Mheshimiwa Freeman Mbowe alimpongeza Rais Kikwete kwa uchapaji kazi ambao umewezesha nchi kuwa na miondombinu bora ikiwemo ya barabara.

“Mimi ninasafiri karibu nchi nzima kwa njia mbalimbali yaani ndege na magari,jamani mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni,Rais Kikwete anastahili kupewa sifa kwa kazi kubwa anayoifanya.

Mbunge huyo wa Hai pia alitumia firsha hiyo kutoa ombi kwa Rais Kikwete la kuongeza kipande cha urefu wa barabara hiyo kwa kilometa nne ili kiweze kuunganishwa na barabara nyingine ya Machame.

Kadhalika Mheshimiwa Mbowe alimuomba Rais kuingilia kati madai ya fidia ya wananchi wapatao 390 waliokuwa wanamiliki ardhi katika mji wa Bomang’ombe ambao waliamishwa kwa ajili nya kujengwa kwa mji huo ambao ni makao makuu ya wilaya ya Hai.

RATIBA YA TUME YA KURATIBU MAONI YA KATIBA

Posted by MK On 00:13 No comments

RATIBA YA TUME YA KURATIBU MAONI YA KATIBA KATIKA WILAYA YA  HAI
TAREHE

MUDA
KATA HUSIKA
KATA ZA NYONGEZA
KITUO CHA MKUTANO
21/10/2012
03:00 – 06:00
HAI MJINI
MASAMA KUSINI
DOUBLE ROAD
21/10/2012
08:00 – 11:00
MASAMA RUNDUGAI

SOKONI
22/10/2012
03: 00 – 06:00
MACHAME KUSINI
MACHAME WERUWERU
MAILI SITA
22/10/2012
08:00 – 11:00
MACHAME MASHARIKI
MACHAME NARUMU
LYAMUNGO KATI
23/10/2012
03:00 – 06:00
MACHAME MAGHARIBI
MACHAME UROKI
BWANI
23/10/2012
08:00 – 11:00
MACHAME KASKAZINI

BARAZANI
24/10/2012
03:00 – 06:00
MASAMA MASHARIKI
MASAMA KATI
MUDIO
24/10/2012
08:00 – 11:00
MASAMA MAGHARIBI

LUKANI




BIBI WA KIJERUMANI AIPIGA JEKI SHULE YA MSINGI CHEMKA

Posted by MK On 10:07 No comments

 Bibi Elisabeth Dorr akipokeza zawadi ya kitenge na mkeka kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Chemka
 Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga mara baada ya kupokea majengo ya shule ya msingi ya Chemka yaliyofadhiliwa na Bibi Elisabeth Dorr.Wengine katika picha ni mkurugenzi wa Shirika la AKO-Moshi, Klaus Peter Kiefe(wa saba kulia),mwalimu kutoka Ujerumani Barbara(wa sita kutoka kulia) na Oscar wa tatu kulia.
 Mgeni rasmi katika hafla ya kupokea majengo ya shule ya msingi ya Chemka Novatus Makunga akiwa na washirika wa maendeleo kutoka Ujerumani wakiongozwa na Bibi Elisabeth Dorr
 Sehemu ya jengo la bwalo la chakula la shule ya msingi ya Chemka lililojengwa na bibi Elisabeth Dorr
 Mabenchi na meza katika bwalo la chakula shule ya msingi ya Chemka
 Bibi Elisabeth Dorr akikumbatiana na baadhi ya akinamama wa kijiji cha Chemka baada ya kufurahishwa na zawadi mbalimbali


Na Richard Mwangulube,Hai

Shule ya Msingi ya Chemka iliyopo nje kidogo wa mji wa Bomang’ombe wilayani Hai,mkoani Kilimanjaro imepokea majengo yaliyojengwa na Bibi Kizee wa Kijerumani Elisabeth Dorr(89) kupitia shirika la Ako lililoko mjini Moshi.

Shule hiyo iliyopo katika kijiji cha Chemka ilipata ufadhili huo mwaka 2008 kupitia kanisa katoliki parokia ya Chekereni kupitia shirika la AKO-Moshi

Majengo hayo ni pamoja na madarasa matatu,nyumba mbili za walimu,bwalo la chakula,stoo na ofisi ya shule pamoja na kugharamia uunganishaji wa umeme na kuvuta maji ya bomba ambapo Bibi Dorr alitoa jumla ya Euro 50,000 ambazo ni sawa na shilingi 93,554,698.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo,David Mosha ameeleza kuwa Bibi huyo wa Kijerumani pia katika fedha hizo alitoa madawati 66,meza 4,viti 4,makabati 7 ya ukutani,sufuria mbili kubwa,beta stoves 2,meza na benchi 15 kwa ajili ya matumizi ya bwalo

Mosha ameeleza kuwa awali Bibi huyo alijenga darasa moja mwaka 2008 na baadaye mwaka uliofuata alimtuma mwenyekiti wa Shirika la AKO-Tanzania,Klaus Boehme na kufurahishwa na usimamizi wa miradi hiyo shuleni hapo.

Aidha Mosha ameeleza kuwa mkuu wa AKO-Moshi alitoa michoro ya ramani tatu za ukutani na michoro sita ya somo la sayansi na kibao cha shule vikigharimu shilingi 800,000/=

Ameeleza kuboreshwa kwa shule hiyo kumeinua kiwango cha ufaulo ambapo mwaka 2008 asilimia 78 waliweza kufaulu,mwaka 2009 asilimia 79,mwaka 2010 asilimia 69 na mwaka jana asilimia 66 huku akieleza kwa mwaka huu wanatarajiwa ufaulu kuwa asilimia 100

Akipokea rasmi miradi hiyo,Mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga amewataka wakazi wa kijiji cha Chemka kuyatunza majengo hayo kwa nguvu zao zote na pia kuhakikisha wanaingia katika kampeni ya kupanda miti kutokana na eneo hilo kunyemelewa na jangwa kutokana na kuwa na idadi kubwa ya mifugo

Aidha Makunga amewataka kutumia fursa ya vyumba bora na vizuri pamoja na umeme kuchangia ununuzi wa kompyuta kwa ajili ya kuanzisha darasa la kompyuta pamoja na kurahisisha kazi za utawala.

Aliahidi kuchangia kompyuta moja kwa ajili ya kuanzia na kuongeza kuwa siyo kwamba kukiamilika kwa majengo hayo kutaifanya shule hiyo kufanana na shule za mjini lakini pia kutawaingia katika mazingira ya kisasa ya teknolojia zinazotumika katika maeneo ya mjini





RC GAMA AZITAKA HALMASHAURI KUFUFUA ZAO LA KAHAWA

Posted by MK On 23:24 No comments

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe Leonidas Gama(Mwenye suti ya Kijivu) akipata maelezo ya utafiri wa miche bora ya kahawa kutoka kwa wataalamu wa Tacri
Mmoja kati ya wafanyakazi wanaosaidiana na wataalamu wa Tacri katika kuzalisha miche bora ya Kahawa
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe Leonidas Gama akishuhudia baadhi ya miche iliyozalishwa na Tacri ikiwa  tayari kwa ajili kwa ajili ya kusambazwa kwa wakulima kwa ajili ya kuoteshwa
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Leonidas Gama(Katikati) na mkuu wa wilaya ya Hai,Mhe Novatus Makunga(kulia) akipata maelezo kuhusiana na msitu wa asili unaotunza na Tacri kutoka kwa mtaalamu wa taasisi hiyo


Na Mwandishi Wetu,Hai

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Mhe Leonidas Gama ametangaza mkakati maalumu wa kufufua zao la kahawa katika mkoa huo kwa kuitumia ipasavyo Taasisi ya utafiti wa Kahawa Nchini(TACRI) ambayo ipo wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro.

Mkuu huyo wa mkoa ametoa kauli hiyo katika ziara yake wilayani Hai ambapo katika ziara hiyo ya siku tatu alipata fursa ya kutembelea taasisi hiyo na kujionea shughuli mbalimbali za utafiti wa zao la Kahawa.

Mhe. Gama ameeleza kuwa halmashauri zote saba za wilaya katika mkoa wa Kilimanjaro zitalazimika kuandaa mkakati wa kukitumia kituo hicho katika kufufua zao la kahawa ambalo kilimo chake kimeporomoka sana mkoani humo.

“Ukizungumzia Kilimanjaro ni kahawa na ukizungumzia kahawa ni Kilimanjaro hivyo ni vyema sasa tukaja na mkakati kabambe wa kufufua zao hilo kwa ajili ya kuinua uchumi wa wananchi wetu,mkoa na taifa kwa ujumla,”alisisitiza

Mhe. Gama ameeleza kuwa tayari wilaya kama ya Mbinga mkoani Ruvuma imeweza kuinua zao la Kahawa kutokana na halmashauri ya wilaya hiyo kukitumia vyema kituo cha utafiti wa kahawa kilichoko wilayani humo.

DC HAI,ALIKOTOKA NA ALIKOPITIA

Posted by MK On 15:27 No comments

2002-National Executive Committee Member, Daniel Ole Njoolay who is also Arusha’s Regional Commissioner congratulating Novatus Makunga (left) after being elected publicity secretary of the Party in Arusha region. The CCM regional conference was held in Arusha recently

DC WA HAI ATEMBELEA SOKO LA RUNDUGAI

Posted by MK On 20:52 No comments




Na Richard Mwangulube

Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga ameuagiza uongozi wa kata ya Masama Rundugai kuhakikisha wanakaa na wakala anayelisimamia soko na Rundugai kwa lengo la kutatua kero zilizoko ndani ya mamlaka yao wakati mipango ya uboreshaji wa soko ikisubiri mikakati  ya halmashauri ya wilaya.

Makunga ametoa agizo hilo baada ya kutembelea soko hilo ambalo hufanyika mara moja kwa wiki yaani kila jumatatu.

Baada ya kutembelea soko hilo na kukutana na maofisa mbalimbali wa kata ya Masama Rundugai na kijiji cha Rundugai,aliwataka viongozi hao kutatua tatizo la matumizi ya choo ambacho wananchi walidai kuwa kinafungwa muda wote na funguo hazifahamiki zinahifadhiwa wapi pamoja na ukosefu wa maji.

Wananchi wanaotumia soko hilo wameeleza kuwa wanalazimika kwenda kujisaidia maporini kandokando mya reli inayokatisha jirani na soko hilo na pia wamelalamikia huduma ya maji kwa madai ya kwamba wanatumia ya mwananchi jirani kwa kuwa soko hilo halina maji.

Makunga ameeeleza kero ya choo ambacho tayari kipo pamoja na kuvutwa kwa maji limo ndani ya uwezo wa uongozi wa kijiji na kata pamoja na wakala anayesimamia soko hilo huku akiongeza kuwa mipango ya kuliboresha soko hilo ikiwa jukumu la halmashauri ya wilaya ya Hai.

Ameeleza kuwa baadhi ya mikakati ambayo ni lazima ichukuliwe ni pamoja na kuondokana na utaratibu wa kupanga bidhaa chini ya ardhi pamoja na kujenga mazingira mazuri ya ufanyaji wa biashara na shughuli nyingine katika soko hilo.

Wananchi wa eneo hilo wameeleza kuwa soko hilo ni la muda mrefu sana ambapom pamoja na kulipa ushuru wa kati ya shilingi mia tatu na mia tano lakini hakuna uboreshaji wowote unaofanyika.

HAI VILLAGE LEADERSHIP SUSPENDED

Posted by MK On 09:10 No comments



 
Monday, 17 September 2012 08:33

By The Citizen Reporter,Moshi.

The entire leadership of Kwa Saadala, a sprawling village along the Arusha-Moshi highway, has been suspended over alleged embezzlement of  public funds and illegal sale of village assets.

The order was given over the weekend by the Hai District Commissioner, Mr Novatus Makunga, who said a probe team would be formed to investigate allegations that a public land meant for social and community services, such as schools, has been sold to individuals.Accused village leaders have been directed to step aside, as the probe into the scam gets underway. 

Those suspended include the Village chairman, Mr Ernest Munisi, Village Executive officer, Mr Claire Ramadhani and Masama South Ward Executive officer. A six-member team comprising officials from Moshi District Council, including the Land officer, Legal officer, Internal auditor, Personnel officer, Administrative officer and Supplies officer, will investiage the scam and has been given one week to complete the task.

Mr Makunga said that once the team completes its task, a meeting would be convened for all village stakeholders to discuss the findings of the report and what should be done to those proved guilty and have cases to answer. 

At last weekend's meeting, most residents alleged that the village chairman was behind the sale of the public land. One of them, Ms Judica Swai, claimed that open spaces close to the Msamadi Primary School had also been sold  without the school management and villagers’ consent.