NAFASI 24 ZA KAZI WILAYANI HAI

Posted by Arusha by day and by night On 06:18 No comments



NAFASI ZA KAZI

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA HAI

MASHARTI YA JUMLA KWA WAOMBAJI WOTE

Ø  Awe raia wa Tanzania na mwenye umri usiozidi miaka 45
Ø  Waombaji wote waambatanishe vyeti vya kuzaliwa
Ø  Waombaji waambatanishe maelezo binafsi yanayojitosheleza(detailed CV) yenye anuani na namba ya simu za kuaminika na majina ya wadhamini(Referees) watatu wa kuaminika.
Ø  Maombi yaambatanishwe na vivuli vya vyeti vya taaluma,picha za Passport size mbili,maelezo,nakala ya vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofika kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika.Viambatanishi hivyo vibanwe vizuri kuondoa uwezekano wa kudondoka au kupotea.
Ø  Tesmonials,provisional Results”Statement of result” hati ya matokeo ya kidato cha nne na sita(Form IV and Form VI Result Slips) havitakubaliwa.
Ø  Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika (TCU na NACTE)
Ø  Waombaji ambao tayari ni watumishi wa umma na wamejipatia sifa za kuingia kutoka kada tofauti na walizonazo,wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao.
Ø  Waombaji waliostaafishwa katika utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wana kibali cha katibu mkuu kiongozi

1.    KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III (NAFASI 4)

SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV waliohudhuria mafunzo ya Uhazili na kufaulu mtihani wa hati ya tatu.Wawe wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja na wawe wamepata mafunzo ya kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuwa na serikali na kupata cheti katika program za Windows,Microsoft Office,Internet,E-Mail na Publisher.

2.    MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II (NAFASI 2)

SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne wenye cheti cha utunzaji kumbukumbu katika fani ya masjala.

3.      MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III (NAFASI 18)

SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye elimu ya kidato cha nne(IV) au sita (VI) aliyehitimu mafunzo ya Astashahada/Cheti katika moja ya fani zifuatazo: Utawala,Sheria,Elimu ya jamii,Usimamizi wa fedha,Maendeleo ya jamii na sayanzi ya sanaa kutoka chuo cha serikali za Mitaa Hombolo,Dodoma au Chuo chochote kinachotambuliwa na serikali.

BARUA ZITUMWE KUPITIA POSTA KWA ANUANI IFUATAYO:

MKURUGENZI MTENDAJI,
HALMASHAURI YA WILAYA
S.L.P 27
HAI

MWISHO WA KUPOKEA MAOMBI NI TAREHE 11/02/2015

0 comments:

Post a Comment