VIJIJI VITANO WILAYANI HAI KUPATA MAJI IFIKAPO SEPTEMBA 30 MWAKA HUU

Posted by Arusha by day and by night On 04:45 No comments

m
Moja ya tanki linalopeleka maji katika kijiji cha Mbatakero

Na Mwandishi Wetu Hai

Wilaya ya Hai itakamilisha ufikishaji wa maji safi na salama katika vijiji vitano kupitia mkakati wa sasa wa serikali wa Mfumo mpya unaolenga kuleta mapinduzi ya kijamii nchini wa usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo unaojulikana kama matokeo makubwa sasa yaani “Big Results Now” ifikapo Septemba 30 mwaka huu.

Vijiji hivyo vitano kati ya kumi ambavyo kwa kila Halmashauri nchini itahakikisha vinaingizwa katika mpango wa kupata huduma ya maji safi na salama ni Mbatakero,Ngosero,Kwasadala,Kimashuku na Kwatito ambavyo vitaunganishwa na maji safi na salama ya Bomba kutokea katika Skimu ya Lyamungo-Umbwe.

Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akizungumza katika mikutano mbalimbali ya vijiji vya Ngosero na Mijongweni mwishoni mwa wiki ameeleza kuwa maji hayo yatafika kwa umbali wa kilometa 22.73 na utekelezaji wa kazi umefikia asilimia 85.

Ameanisha kazi ambazo tayari zimeshakamilika ni pamoja na ujenzi wa chemba ya kuchukulia maji,ujenzi wa kivuko kutoka mto kikafu,ujenzi wa matanki mawili ya lita za ujazo 50,000 kila moja,ujenzi wa vilula 20,kuchimba mtalo kilometa 21,kulaza na kufukia mambomba kilometa 20

Amewahakishia wananchi wa vitongoji viwili ambavyo viliachwa katika mradi huo vya Landi na Jitengene katika kijiji cha Ngosero nao watapata maji ifikapo mwishoni mwa mwezi Septemba

Amefafanua kuwa katika mpango huo kijiji cha Kimashuku kitahusu vitongoji vya Kinyalu na Kiangaa,Kijiji cha Kwasadala kitongoji cha Faraja na kijiji cha Kwatito ni kitongoji Kasendero

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutaweza kupatikana kwa huduma ya maji kwa wakazi zaidi ya 3,443 katika umbali uziozidi mita 400.

Makunga amesema baada ya kukamilika kwa awamu hiyo ya kwanza,serikali wilayani humo itaanza mara moja utekelezaji wa awamu ya pili ya upelekaji wa maji katika vijiji vitano ambayo inatakiwa kukamilika ifikapo mwezi Juni mwakani.

Ametaja vijiji vitakavyohusika na awamu ya pili kuwa ni pamoja na Sanya Stesheni,Chemka,Mtakuja na Tindigani pamoja na mji wa Bomang’ombe kupitia Skimu ya maji ya Losaa-Kia

“Hivi vijiji vya awamu ya pili vilikuwa na tatizo kubwa sana la maji kwa muda mrefu kutokana na kukosa kabisa chanzo chochote chenye maji safi na salama kutokana na maji ya maeneo hayo kuwa na kiasi kikubwa cha madini ya floride ambayo yamekuwa na athali kubwa kiafya kwa watumiaji na hasa watoto wadogo,”amefafanua

Akifafanua kuhusiana na mji wa Bomang’ombe,Makunga ameeeza kuwa hivi sasa unakabiliwa na uhaba wa maji kutokana na ongezeko kubwa na la kazi la watu kutokana na wenyeji wengi wa mji ya Moshi,Arusha,Mererani na Sanya juu kupenda kuweka makazi yao katika mji huo.

Ameeleza kuwa mji wa Bomang’ombe unaopata maji kutoka skimu ya Uroki-Bomang’ombe ilisanifiwa kwa kutoa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wapatao 10,000.

Kutokana na ongezeko la wakazi wa mji wa Bomang’ombe na kufikia 34,000 kwa sasa,huduma ya maji safi na salama katika mji huo haikidhi matumizi kwa wakazi kwa siku.

Maeneo yenye upungufu wa maji katika mji huo ni Bomani juu na hususani hospitali ya wilaya ambayo kwa kipindi cha kiangazi inapata huduma ya maji wakati wa usiku tu.

WILAYA YA HAI YAINGIA USHIRIKIANO WA MAENDELEO NA SWEDEN

Posted by MK On 01:44 1 comment

Mratibu wa mipango ya maendeleo ambaye pia ni diwani katika manispaa ya Arvidsjaur,Stina Johansson(tatu Kulia) akiwa na ujumbe wa viongozi kutoka wilayani Hai-kutoka kulia,Novats Makunga(Mkuu wa wilaya),Clement Kwayu(Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya),Melkizedeck Humbe(Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri) na Ester Mbatiani ambaye ni afisa mipango mkuu wa Halmashauri
 Watendaji wa Manispaa ya Arvidsjaur na halmashauri ya wilaya ya Hai wakibadilishana mkataba wa ushirikiano
 Viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Hai na wale wa Manispaa ya Arvidsjaur katika kusainiana makubaliano ya ushirikiano
Meya wa manispaa ya Arvidsjaur,Jerry Johqnsson(Katikati) akifafanua jambo baada ya kumalizika itifika ya kusaini makubaliano na hamashauri ya wilaya ya Hai,anayeshuhudia ni mwenyekiti wa halmashauri Clement Kwayu


Na Richard Mwangulube,Hai


Halmashauri ya wilaya ya Hai,imeingia mkataba wa miaka minne wa ushirikiano na Manispaa ya Arvidsjaur  nchini  Sweden  unaolenga katika maeneo ya kiuchumi na kijamii ukiwemo wa teknolojia ya kisasa ya udhibiti wa takataka kiuchumi kwa kuziwezesha kutengezwa upya bidhaa kwa ajili ya matumizi



Mkataba huo ulitiwa saini  wakati wa ziara ya ujumbe wa viongozi  wa wilaya ya  Hai uliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya Hiyo, Novatus Makunga hivi karibuni katika  makao Makuu ya Manispaa hiyo nchini Sweden.



Wajumbe wengine Katika ziara hiyo ya siku tano ambao ndiyo waliosaini mkataba huo ni pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Wilaya ya Hai Clement Kwayu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Melkizedeck Humbe pamoja na Afisa Mipango   wa Halmashauri Ester Mbatian



Kufuatia  mkataba huo, Halmashauri ya Wilaya ya Hai itapaswa  kuandaa na kuwasilisha katika Manispaa ya Arvidsjaur  miradi mbalimbali inayolenga katika Nyanja za biashara na  viwanda vidogo na vya kati



Maeneo mengine ya shirikiano huo ni pamoja na  elimu na utoaji wa taarifa, uboreshaji   na usimamizi  wa mazingira endelevu pamoja na miradi inayolenga   masuala ya  ajira  kwa vijana.



Akizungumza na waandishi wa habari mjini Hai mwishoni mwa wiki,Makunga  amesema kadhalika ushirikiano ho unalenga  katika kuimarisha  shughuli  mbalimbali zinazohusiana na masuala ya sekta ya utalii na utawala bora kuanzia ngazi ya chini kabisa.



“Kwa kushirikiana na wenzetu tunaandaa mkakati wa kuimarisha mafunzo kwa  jamii katika masuala ya uchumi na  shughuli za maendeleo ya Kijamii na lengo kubwa zaidi ni kwa kundi la vijana”. Amefafanua Makunga



Ameeleza kupitia Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Sweden[SIDA] ushirikiano huo pia   utatoa fursa kwa Manispaa ya Arvidsjaur kushirikiana na wilaya ya Hai katika ujenga uwezo kwa halmashauri juu ya namna ya kupata taarifa mbalmbali za maendeleo  na kiuchumi kutoka maeneo ya vijijini nakuzifanyia kazi.



Amesema pia ushirikiano huo umelenga katika kuhakikisha halmashauri ya Hai inaingia katika mfumo wa kisasa wa namna ya kusimamia  ukusanyaji wa mapato na matumizi ya fedha za maendeleo, kuboresha mawasiliano na wadau mbalimbali  ikiwemo kupitia kituo cha halmashauri hiyo cha redio  Boma FM



Amesemasa Manispaa  hiyo ya Sweden  itasaidia  katika ujenzi,uboreshaji na uendelezaji wa  kituo cha  mafunzo kwa ajili ya  maendeleo ya jamii katika wilayani Hai pamoja na kusaidia  katika kuboresha huduma za afya



Masuala mengine yatakayotekelezwa  kutokana na mahusiano hayo  ni pamoja na Manispaa ya Arvidsjaur kusaidia katika teknolojia ya urudufishaji wa taka ambapo unawezesha taka ngumu na taka maji kuweza kutumika tena.



Makunga amesema kuwa suala la udhibiti wa takataka ni changamoto kubwa katika mji wa Hai ambao hauna dampo huku kukabiliwa na ongezeko la kasi la watu wanaopenda kuweka makazi ya kuishi na kuendesha shughuli zao za kazi Arusha,Moshi,Siha na Simanjiro.



“Kwa wenzetu taka ni rasilimali, inachambuliwa kuanzia ngazi ya familia na kupelekwa eneo la kutupa taka, kwa kupangwa kuangalia na aina, na hutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali vikiwemo vikombe, vijiko, sahani na umeme pamoja na mafuta ya kulainishia vyuma kutumika upya,”amefafanua



Ametaja mengine ambayo yatatiliwa mkazo kutokana na ushirikiano huo ni pamoja na  Manispaa hiyo kusaidia katika kukuza uchumi na kuimarisha miundo mbinu ya kiuchumi.



Makunga ameeleza kuwa manispaa hiyo ambayo inamiliki uwanja wa ndege wa kimataifa imeonyesha kuvutiwa kusaidia uimarishaji wa  uwanja wa kimataifa wa Kilimanjaro(KIA)  uliopo wilayani Hai kwa kuongeza  shughuli za  biashara za Anga pamoja na kuboresha miundo mbinu katika Uwanja huo



Ujumbe huo uliweza kupata taarifa juu ya shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Manispaa hiyo zikiwemo za kuchumi, kijamii pamoja na usimamizi bora  wa ukusanyaji na matumizi ya Mapato



Kwa mujibu wa nchi ya Sweden, Mamlaka zote  za Serikali za Mitaa zinajulikana kama Manispaa zinaongozwa kwa sheria ya bunge la nchi hiyo ambapo hivi sasa kuna Manispaa zipatazo 260 nchini Sweden



Manispaa hizi zinawajib wa kusimamia  masuala ya  elimu kuanzia ngazi ya chekechea hadi Sekondari pamoja na kujenga na kusimamia vituo vya malezi ya  wazee na wasiojiweza



Kadhalika manispaa hizi zinawajibu wa  kusimamia vituo vya zimamoto na uokoaji,kusimamia ujenzi  na uendeshaji  wa viwanja vya ndege,kusaidia walemavu pamoja na kuunganisha wajiri na waajiriwa


Pia Makunga ameeleza kuwa Manispaa hizi zinajukumu la kusimamia vituo vya  elimu ya ujasirimali kwa vijana na masuala ya Utalii ambapo  Sweden kila siku hupokea watalii zaidiya 500,000 wanaotembelea vivutio mbalimbali katika Manispaa hizo kutoka nchi za ulaya

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                     


MATENGENEZO YA BARABARA WILAYANI HAI KWA MWAKA WA FEDHA WA 2013/2014

Posted by MK On 22:39 No comments



HALMASHAURI YA WILAYA YA HAI IMEIDHINISHIWA JUMLA YA SHILINGI 460,810,000 KUTOKA MFUKO WA BARABARA.FEDHA HIZI ZITATUMIKA KATIKA MATENGENEZO YA KILOMETA 178.13 ZA BARABARA ZA WILAYA KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014 KAMA IFUATAVYO ;

NOTE: Ni matengenezo ya barabara zilizopo katika ngazi ya wilaya


1.      1: Matengenezo ya kawaida



Km.149.43 kwa Tshs 175,720,000 kwa barabara za:      

No.
BARABARA
KILOMETA
FEDHA
01
Bomang’ombe – Kikavuchini
15.0                 
18,000,000/=
02
Kwasadala – Longoi
14.3                 
17,160,000/=
03
Hai Town Roads                     
12.0                 
14,400,000=
04
Mferejini – Kimashuku             
4.0                   
4,800,000/=
05
Kimashuku – Kwa Tito              
8.0                   
9.600,000/=
06
Ngaya – Kitayiye                        
2.5                   
3,000,000/=
07
Mungushi-Kware                       
3.2                   
3,840,000/=
08
Lambo – Makoa                         
3.7                   
4,440,000/=
09
Lyamungo Sinde – Makoa        
6.0                   
7,200,000/=
10
Kwasadala – Uswaa                   
 8.7                   
10,440,000/=
11
Shirinjoro-Lyamungo Sinde      
13.4                  
16,080,000/=
12
Shirinjoro – Mijongweni           
9.6                    
11,520,000/=
13
Marukeni – Kyuu                        
 9.13                 
10,960,000/=
14
Mbweera – Ufishi                      
 1.4                     
1,680,000/=
15
Kwa Frank – Kyuu                      
8.0                    
9,600,000/=
16
Masama Mulla – Machame Barazani      
3.1                    
3,720,000/=
17
Sonu – Saawe                             
6.0                     
3,600,000/=
18
Lukani – Mashua                        
8.0                    
9,600,000/=
19
Kwasadala – Marukeni              
3.1                     
3,720,000/=
20
Kyuu – Lukani                              
6.0                     
 7,200,000/=
21
Mferejini – Two Bridge              
1.3                    
1,560,000/=
22
Lyamungo Sinde – Mfoni          
3.0                    
3,600,000/= 



1.      2: Matengenezo ya kawaida



              Km. 20 Kwa Tshs. 100,000,000/= kwa barabara za;

Na
BARABARA
KILOMETA
KIASI CHA FEDHA
01
Kyuu  -  Lukani                              
2.0                      
10,000,000/=
01
Kalali – Nroanga                            
4.0
20,000,000/=
03
Bwani – Kyeeri                               
4.0                         
20,000,000/=
04
Aliwasali – Kware                          
4.0                        
20,000,000/=
05
Hai Town Roads                            
4.0                        
15,000,000/=
06
Lambo – Makoa                             
 3.0                        
15,000,000



1.      3: Matengenezo ya muda maalumu [Periodic Maintanence]


Km 8.7 kwa Tshs 135.200,000/=

Na.
BARABARA
UREFU KWA KILOMETA
KIASI CHA FEDHA
 01
Hai Towan Roads                             
2.0                       
32,000,000/=
 02
KIA – Mtakuja                                    
3.1                       
49,600,000/=
 03
Kwa Mengi – Kyalia                          
2.0                      
32,000,000/=
 04
Rundugai - Chemka
1.6
21,600,000/=



1.      4: Ujenzi wa Kalvati/Drift



Ujenzi wa kivuko[drift] moja na ukarabati wa daraja kwa Tshs 27,890,000/=



Ø  Drift 1 – Rundugai – Chemka                                               : Tshs.  19,000,000/=

Ø  Daraja la Semira                                                                    : Tshs     8,890,000/=



1.      5: Usimamizi na matengenezo ya gari                                                     : Tshs.   22,000,000/=