WALIOKUMBWA NA MAAFA WILAYANI HAI WAENDELEA KUPOKEA MISAADA YA UJENZI

Posted by Arusha by day and by night On 06:49 No comments





Na Richard Mwangulube,Bomang’ombe

Wakazi wa kata 8  na vijiji 21  wilawayani Hai  mkoani Kilimanjaro walio kumbwa na maafa ya kuezuliwa  mapaa ya nyumba zao kutokana na upepo mkali ulio ulioambatana na mvua  wameshauriwa kujenga nyumba imara  ambazo zitaweza kuhimiri  hali kama hiyo endapo itajitokeza tena.

Rai  hiyo imetolewa katika vijiji vya Kwatito,Mijongweni na Ngosero vilivyopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro  na mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga wakati wa kukabidhi msaada wa mabati yenye thamani  ya shilingi milioni 5.2.

Msaada umetolewa na Kampuni ya Megatrade Investment Limited ya Arusha baada  ya kuguswa na maafa hayo,ambapo Makunga amesema , kutokana na maafa ya namna hiyo kujirudia kila mwaka ni vyema sasa wakazi wa vijiji hivyo wakajenga nyumba imara kwa kutumia matofali ya kuchoma.

Ameeleza kuwa eneo la vijiji hivyo vina udongo mzuri unaofaa kwa matofali ya kuchoma na kwamba sasa wakati umefika wa viongozi kuanza kampeni ya kuhamasisha wananchi kuyatumia matofali hayo kwa ujenzi.

Amesishukuru kampuni hiyo kwa kukubali kutoa msaada kwa waathirika hao ambao wengi wao itawachukuwa muda mrefu kurejesha nyumba zao na kurudi kwenye makazi yao kutokana na hivi sasa kujihifadhi kwa majirani.

Makunga ameeleza kuwa serikali imeshatoa msaada wa chakula tani 45.7 ambapo kila mtu aliyeathirika na maafa hayo amepatiwa kilo 35 ambaz zitamtosheleza kwa kipindi cha miezi mitatu.

Amesema kuwa awali walitoa kilo ishirini wa unga wa sembe na kilo tano za Maharage kwa kila kaya kutokana na msaada kutoka kampuni ya Bonite Bottles ya Moshi,kiwanda cha unga cha Monaban cha Arusha na makampuni ya mahoteli ya Serena.

Kwa upande wake meneja masoko wa Kampuni ya Megatrade,Gudlack Kway amesema  wameguswa na maafa hayo na  kwa kuwa kampuni yao hufanya kazi Zaidi katika jamii ndio maana wameamua kutoa msaada wa mabati hayo ambayo yatawasaidia waathiriwa katika ujenzi wanaotarajia kuuanza muda si mrefu.

Mwishoni mwa mwezi Februari  wilaya ya Hai kwa nyakati tofautitofauti ilikumbwa na  upepo mkali ulio ambatana na mvua kubwa  iliyo sababisha maafa katika vijiji 25 ikiwemo kuezuliwa kwa mapaa ya nyumba,kubomoka kwa kuta za nyumba kuharibika kwa mazao shambani na  kifo cha mtu 1 katika kijiji cha Kwatito

0 comments:

Post a Comment