KAMATI YA BUNGE YA ULINZI NA USALAMA YATINGA KILIMANJARO

Posted by Arusha by day and by night On 02:54 1 comment


Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi (MPA) zamani kikijulikana kama CCP), Matanga Mbushi (kulia) akiwatembeza chuoni hapo wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama walipo fanya ziara chuoni hapo juzi.

SERIKALI YAANZA KUSAMBAZA MSAADA WA CHAKULA WILAYANI HAI

Posted by Arusha by day and by night On 23:53 No comments



Na Richard Mwangulube,Hai

Serikali wilayani Hai imeanza kusambaza chakula cha msaada kwa kaya 8,402 zenye upungufu wa chakula wilayani humo.

Mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake amethibiisha kuanza kwa zoezi hilo la usambazaji wa mahindi Jumatano iliyopita.

Hata hivyo Makunga amezionya kamati za maafa za vijiji zinazohusika kuwatambua wahitaji wa msaada huo kuwa na uadilifu kwa kuhakikisha kaya zinazostahilika msaada huo inaidhinishwa na mikutano mikuu ya vijiji.

“Maelekezo ya jinsi ya kusimamia zoezi hilo yapo wazi na wahusika katika ngazo zote za chini yanayafahamu na tumewapelekea kimaandishi hivyo hatutasita kumchukulia hatua kiongozi yeyote atakayekiuka muongozi uliotolewa kwa maslahi binafsi,”alisisitiza makunga

Aidha mkuu huyo wa wilaya amezitaka kaya ambazo zilifanikiwa kuvuna chakula cha kutosha katika msimu uliopita wa kilimo kuhakikisha zinahifadhi chakula cha kutosha hadi msimu huu wa kilimo unaotarajiwa kuanza mwezi April.

Makunga ameeleza kuwa msaada huo mahindi tani 201.6 yametoka ofisi ya waziri mkuu na kupitia katika maghala ya Wakala wa hifadhi ya chakula nchini(NFRA) yaliyopo jijini Arusha.

Makunga ameeleza kuwa jumla ya kaya 7,561 zitanunua mahindi hayo kwa bei nafuu ya shilingi 50 kwa kilo huku kaya 841 zizokuwa na uwezo zitapewa msaada huo bure.

Ameeleza kuwa kila kaya itapata kilo 24 ambazo zitatosha kwa matumizi ya miezi miwili.

Makunga ameeleza jumla ya vijiji kumi na viwili na mitaa sita itanufaika na msaada huo wa chakula.

Amevitaja vijiji hivyo kuwa ni pamoja na Mtakuja,Tindigani na Sanya Stesheni(kata ya Kia),Mkalama(kata ya Masama Rundugai),Mbatakero na Kwatito katika kata ya Machame Kusini.

Vijiji vingine ni Longoi na Ngusero(Machame Weruweru),Usari,Tella na Mulama(kata ya Narumu) na Kitongoji cha Lambo kilichopo kata ya machame Kaskazini.

Kwa upande wa mitaa iliyopo katika kata ya Hai mjini ameitaja kuwa ni pamoja na Lerai,Kilimambogo,Mlima Shabaha,Kambi ya Nyuki,Gezaulole na Kambi ya Raha.