UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM YA MWAKA 2005 HADI 2012 KATIKA WILAYA YA HAI

Posted by MK On 09:03 No comments



TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM 2005 HADI 2012  KATIKA WILAYA YA HAI KWA AJILI YA PROGRAMU MAALUMU KWA VYOMBO VYA HABARI

UTANGULIZI

Awali ya yote nianze kuwatakia heri ya mwaka mpya wananchi wote wa wilaya ya Hai.

Mwaka 2013 ndiyo kwanza umeanza,ni matarajio yangu kwamba utakuwa mwaka wenye shughuli nyingi na pilika pilika nyingi sana na kila mmoja wetu atajituma zaidi katika kuhakikisha ana boresha hali ya maisha yake,wilaya na taifa kwa ujumla

Mwaka uliopita yaani wa 2012 haukuwa mzuri sana kwetu wilaya ya Hai kutokana na kuendelea kukosa mvua za vuli pamoja na masika na  ikiwa ni  mwendelezo wa hali hiyo kujitokeza mfululizo katika miaka ya karibuni.

Tunamshukuru mungu kwa mwaka huu kidogo kumekuwepo na ahueni katika mvua tumebahatika  kupata mvua za vuli ambazo zimeendelea kunyesha kuanzia katikati ya mwezi Desemba mwaka jana mpaka hii Januari.

Wananchi wenzangu wa wilaya ya Hai nimekuja leo katika kituo chetu cha Radio cha Boma FM kwa lengo moja nalo ni kuzungumzia ahadi zilizotolewa na serikali yenu iliyopo madarakani kupitia ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya  mwaka 2005 hadi 2012

Ni sehemu ya kwanza ya ilani ya mwaka 2005 hadi 2010 pamoja na utekelezaji wa miaka miwili ya ngwe ya mwisho ya serikali ya awamu ya nne yaani mwaka 2010 hadi mwaka jana 2012.

Kama wengi mnavyofahamu ilani ya uchaguzi ni chimbuko la yanayotekelezwa kutokana na ahadi za chama kilichofanikiwa kushika dola baada ya kukamilika kwa uchaguzi mkuu

Kwa hiyo katika uchaguzi mkuu wa kuingiza madarakani serikali ya awamu ya nne mwaka 2005,serikali ambayo ipo madarakani ilikuja na ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2005 hadi 2010.Baadaye ilani ya uvhaguzi ya mwaka 2010 hadi 2015.

Hivyo ilani ya uchaguzi ni maelezo ya sera katika kipindi husika na ilani inalenga kuwaeleza wananchi ni mambo gani chama kilichopo katika kinyang'anyiro cha kushika dola ama uongozi kitafanya iwapo kitashinda uchaguzi na kuunda serikali.

Sera hizo zilibebwa na kunadiwa na wagombea wa ngazi mbalimbali kupitia serikali iliyopo madarakani chini ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na wagombea wengine wa ngazi za  ubunge na udiwani.

Kimsingi ccm ilishinda na kuunda serikali ingawa katika baadhi ya maeneo ilipoteza majimbo kwa kushindwa ubunge na katika sehemu nyingine kata kwa kushindwa udiwani lakini kwa kushinda nafasi ya urais iliunda serikali na hivyo serikali inatekeleza ilani hiyo ya ccm.

Ahadi na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2005 hadi 2012, kimsingi inagusa  katika maeneo yapatayo nane ambayo ni pamoja na  sekta ya uzalishaji mali,sekta ya miundombinu na huduma za kiuchumi,sekta ya uwezeshaji wananchi kiuchumi,sekta ya huduma za jamii, utawala bora,Demokrasi na madaraka yaumma,kuendeleza makundi maalumu pamoja na michezo na utamaduni

Lakini kabla ya kuanza labda niwakumbushe kwamba wilaya yetu ya Hai kwa mwaka 2005 hadi 2010 ilikuwa na kata kumi na vijiji hamsini na vitano tofauti na kuanzia mwaka 2010 hadi 2012 ambapo  baada ya  uchaguzi mkuu wa 2010   wilaya ilipata kata kumi na nne na vijiji sitini.

Wilaya ya Hai ina eneo lenye jumla ya kilometa za mraba 1,011 sawa na asilimia 7.6 ya eneo lote la mkoa wa kilimanjaro ambalo ni kilometa za mraba 13,309 na hivyo kuwa ya tano kwa ukubwa wa eneo kati ya wilaya sita zinazounda mkoa wa kilimanjaro.

Hadi kufikia mwaka 2010 wilaya ilikadiriwa kuwa na wakazi 197,847 kutokana na kuwa na kadirio la ongezeko la asilimia 1.6 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002.msongamano wa watu ni watu 360 kwa kilometa moja ya mraba.

Kutokana na utafiti wa kiuchumi wa mwaka  2005 ulionyesha kuwa pato la mkazi lilikuwa shilingi 540,000 kwa mwaka
1.   SEKTA YA UZALISHAJI MALI
Sekta hii imegawanyika katika maeneo yapatayo manane ambapo ni pamoja na kilimo,umwagiliaji,mifugo,uvuvi,wanyamapori na misitu,utalii na viwanda vidogo na biashara pamoja na ushirika
Kilimo
Tukianza na kilimo,lengo la serikali katika ilani lilikiwa kuhakikisha ukuaji wa kilimo unafikia angalau asilimia ishirini ifikapo mwaka 2010.

Sababu ,Wakazi wengi wa wilaya ya hai hutegemea zaidi shughuli za kilimo kwani zaidi ya asilimia 80 ni wakulima wadogo wadogo wanaojishughulisha na kilimo na shughuli za ufugaji.

Eneo linalofaa kwa shughuli za kilimo linakadiriwa kuwa na jumla ya hekta 46,506.

Katika uchangiaji wa kisekta katika uchumi,kilimo na mazao kinachangia asilimia 51.2 na kwa upande wa pato,kilimo kinachangia kwa asilimia 41.3 huku mifugo na ufugaji katika uchumi ikichangia asilimia 48.8 na kwa pato ikichangia kwa asilimia 40.4.

Sehemu nyingine iliyobaki ya asilimia kama 18.39 inachangiwa na sekta nyingine ambazo ni pamoja na biashara na viwanda,ujenzi,uchukuzi na usafirishaji,huduma za fedha pamoja na utawala.

Mkakati wa utekelezaji wa ilani katika kilimo ulikuwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba wakulima vijijini wanafikishiwa maarifa na kanuni za kilimo bora cha mazao wanayolima na elimu juu ya hifadhi ya udongo.

Lakini pili kuwa na mpango wenye malengo yanayopimika katika kueneza matumizi ya zana bora za kilimo.

Tatu, kuwezesha na kushawishi utengenezaji na upatikanaji wa mikokoteni ya kuvutwa na wanyama na vinu vya kisasa vya kukobolea na kusagishia  nafaka

Na nne kuweka utaratibu wa upatikanaji wa mbegu bora na mbolea na kuimarisha utaratibu wa kutoa ruzuku ya mbolea na kutengeneza mbolea ncini
Tano kuweka utaratibu wa mashindano ya kilimo katika vijiji,kata,tarafa,wilaya na mkoa.

Katika eneo  hilo la kilimo,sehemu kubwa ya ahadi zilitekelezwa katika wilaya ya Hai kwani serikali imeweza kutoa ushauri kwa wakulima 1,382,310 ikiwa ni sawa na wastani wa wakulima 276,462 kwa mwaka na kuanzishwa mashamba darasa 1,023  katika kata zote.

Aidha jumla ya jozi 339 za wanyamakazi zilinunuliwa katika kata tatu za masama kusini,masama rundugai na hai mji kadhalika mikokoteni 80 ilitengezwa na kusambazwa katika kata za Masama Kusini,Masama Rundugai na hai mjini pamoja na vinu vya kusagisha na kukoboa 66 na 11 vya kusindika alizeti vilinunuliwa Kwa kata zote.

Aidha serikali iliteua mawakala wa kusambaza pembejeo wapatao 10 kwa kata zote kwa mwaka 2005 na idadi hiyo kuongezeka na kufikia mawakala 26 mwaka 2012.

Serikali imeendelea kutoa pembejeo za ruzuku mwaka hadi mwaka kwani kwa kati ya mwaka 2005 na 2008 ziliweza kusambazwa jumla ya  mbegu tani 484 na mbolea tani 6,801.

Serikali iliendelea kuongeza kiasi cha pembejeo za ruzuku zikiwemo mbegu na mbolea ya kupandia na mbolea ya kukuzi mwaka hadi mwaka.Mfano katika mwaka 2008/2009 idadi ya vocha zilikuwa 10,870 na kuongezeka katika mwaka 2009/2010 na kufikia 18,600.Mwaka 2010/2011 ili idadi ya vocha 24,728.

Pembejeo hizo ni kwa ajili ya mbegu za mazao ya mahindi na mbunga pamoja na mbolea za kupandia na kukuzia mazao.
Kilimo cha umwagiliaji maji
Kwa upande wa kilimo cha umwagiliaji maji katika eneo hilo ahadi ilikuwa kukarabati mifereji ya asili ipatayo 140 na kujenga matenki ya maji ya mvua yapatayo 30 na kujenga mabwawa 27.

Kimsingi wilaya ya Hai ina eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji la  hekta 27,406 ambazo kati ya hizo ni hekta 17,030 ndizo zinazotumika kwa umwagiliaji.

Wilaya katika utekelezaji wa ilani imeanza kazi ya kukaraba miundombinu ya umwagiliaji kupitia mpango wa maendeleo ya kilimo wilaya yaani DADPs na kuongeza eneo la umwagiliaji hasa katika maeneo ya kata za Machame Kusini,Machame Weruweru,Masama Rundugai na Masama Magharibi.

Mifereji ya asili ilikaratabiwa katika kata sita kati ya kata zote kumi na nne ambazo ni kata za Machame Kusini,Machame Kaskazini,Machame Mashariki,Masama Mashariki,Masama Magharibi,Masama Rundugai na Masama Kusini

Katika mwaka wa fedha wa 2011/2012 wilaya ilikuwa inatekeleza miradi ya maendeleo ya kilimo ipatayo 19 ambapo miradi 16 inatekelezwa chini ya mpango wa maendeleo ya kilimo wilaya yaani DADPs ikiwemo miradi 3 ya umwagiliaji maji iliyotengewa jumla ya shilingi 120,000,000 na miradi mingine 13 iliyotengewa shilingi 192,000,000.Miradi mingine 3 inatekelezwa chini ya mfuko wa uendelezaji umwagiliaji wilaya yaani DIDF kwa jumla ya shilingi 420,000,000.

Aidha katika eneo hilo la kilimo serikali iliahidi kuandaa maofisa ugani wa fani mbalimbali za kilimo na kuwaelekeza wanakohitajika hasa vijijini ambapo jumla ya maofisa ugani 83 walipatiwa mafunzo katika kata zote.

Kilimo cha mazao ya kudumu na biashara
Ilani pia ilihimiza kampeni za kaya kupanda mazao ya kudumu kama michungwa,miembe,mifenesi na mibuni na pia watu wenye uwezo kuanzisha mashamba makubwa ya mazao ya kudumu.

Katika wilaya yetu nguvu kubwa ilielekezwa katika mibuni ambapo mibuni 854,000 imeoteshwa katika kata nane za Machame Mashariki,Masama Mashariki,Masama Magharibi,Masama Musini,Machame Magharibi,Machame Kusini,Machame Uroki na Machame Kaskazini

Aidha katika jitihada za kufufua zao la kahawa,wakulima na serikali kwa maana halmashauri ya wilaya kwa kushirikiana na kituo cha utafiti wa kahawa,TACRI tumeshirikiana katika juhudi za kukuza na kusambaza miche bora ya kahawa inayostahili magonjwa ya Chulebuni na Kutu ya majani.

Zilianzishwa bustani mama za kahawa bora 63 zinazolenga kuzalisha miche bora kati ya 522,120 na 1,014,424 katika kata saba za  Machame Uroki,Machame Kaskazini,Machame Mashariki,Masama Magharibi,Masama Rundugai na Machame Magharibi.

Hata hivyo katika zao la kahawa bado wilaya ina kabiliwa na changamoto kubwa ya kushuka kwa uzalishaji kunakotokana na moja- kushuka mara kwa mara kwa bei katika soko la dunia na hivyo kuwakatisha tamaa wakulima,mbili- gharama kubwa za uzalishaji kutokana na bei kubwa ya pembejeo na zana,tatu -vijana wengi kutopenda kujihusisha na uzalishaji wa zao la kahawa na hivyo mashamba mengi kuachiwa wazee na nne-  mabadiliko ya hali ya hewa.

Takwimu zinaonyesha kwamba uzalishaji huo ulishuka kutoka tani 2,568.3 kwa mwaka 2007/2008 hadi tani 2,061.3 kwa mwaka 2008/2009 na mwaka uliofuata wa 2009/2010 kufikia tani 1,150.

Katika kuongeza mazao yanayoweza kuongeza kipato kwa haraka zaidi pia sera zilielekeza katika kuhimiza kilimo cha maua,matunda,viungo na kilimo cha artemizia.

Kwa ujumla mazao ya biashara yanayolimwa katika wilaya yetu ni pamoja na kahawa,ndizi, alizeti,vitunguu,mpunga na maua.

Jumla ya hekta 427.6 za maua zililimwa huku jumla ya hekta 17 za matunda nazo zililimwa yakiwemo maparachichi na miembe katika kata za Machame Kaskazini na Masama Mashariki.Mashamba ya maua yanaendeshwa na wawekezaji.

Katika kipindi hicho pia msisitizo mkubwa ulikuwa kuhimiza kilimo cha mimea ya mbegu za mafuta na kufufua ama kuanzisha viwanda vya kusindikia mafuta.Jumla ya hekta 2000 za alizeti zililimwa  na kuoteshwa katika kata tatu za Machame Kaskazini,Machame Kusini na Masama Rundugai  pamoja na kartamu katika kata ya Masama Rundugai.

Kwa upande wa viwanda,wilaya yetu ilipata viwanda 11 vya kusindikia mafuta katika kata ya Hai Mjini,Machame Kusini na Machame Kaskaini.

Katika kumalizia eneo hili la kilimo,ilani ilihimiza kuweka mkazo sera ya wilaya kulima mazao kulingana na hali ya hewa itakayowawezesha wakulima kuwa na uhakika wa kuvuna na hapo msisitizo ulikuwa kulima  mtama hekta 436

Katika utekelezaji jitihada kubwa imefanyika kwa  mtama  kulimwa katika kata za Masama Rundugai na Machame Kusini pamoja na muhogo katika kata ya Masama Kusini.

Sekta ya mifugo
Tukitoka hapo katika kilimo,ebu sasa tuangalie sekta ya mifugo,katika mifugo  malengo yaliyoanishwa yalikuwa kuendeleza na kuzingatia ubora wa mifugo kuliko wingi pekee wa mifugo.

Ufugaji katika wilaya ya Hai umegawanyika katika kanda kuu tatu,ukanda wa juu,ukanda wa kati na ukanda wa tambarare.ukanda wa juu na wa kati unafanyika ufugaji wa ndani ambao mifugo hulishwa kwa kutumia nguvu kazi ya familia na vibarua.ukanda wa tambarare kunafanyika ufugaji wa kuchunga ambako kuna idadi kubwa ya ng'ombe wa kienyeji,mbuzi,kondoo na punda.

Mkakati, moja ni pamoja na kufufua na kujenga mabwawa na majosho mapya kwa ajili ya mifugo.

Mbili, kuendelea kutenga maeneo ya wafugaji kwa lengo la kupunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji lakini tatu kuendelea kukuza na kuendeleza masoko ya ndani ya mifugo na mazao yake

Tatu, kuendelea kuhamasisha uimarishaji na uanzishwaji wa vikundi vya ushirika wa wafugaji

Katika kutekeleza wa mikakati hiyo,majosho kumi yalijengwa katika eneo la Masama Rundugai.

kulifunguliwa pia vituo vya afya ya mifugo kumi,kliniki ya mifugo moja,vituo vya kukusanyia maziwa 12,mnada wa mifugo mmoja,mabanda ya ngozi mawili,machinjio moja,visima vya kuchinjia 153,saccos zinazotoa mikopo nne,mabucha 156 na nyumba za watumishi 9.

Kiasi cha eneo la hekta  1,034 lilitengwa kwa ajili ya maeneo ya wafugaji katika kata za Masama Rundugai na Hai mjini.

Kwa upande wa elimu,jumla ya wafugaji 20,130 katika kata zote walipatiwa elimu katika maeneo matatu ambayo ni pamoja na mashamba darasa ya mifugo kwa wafugaji 13,mafunzo darasani wafugaji 20,080 na ziara za mafunzo wafugaji 37.

Aidha elimu ya wafugaji ilitolewa na wataalamu wa mifugo walioko wilayani na vijijini pamoja na watafiti mbalimbali kutoka vituo vya Tengeru Arusha,Chuo Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine Morogoro na Kituo cha utafiti cha Selini cha Arusha.

Jumla ya madume bora 72 yalisambazwa na  ng'ombe 1,100 walihamilishwa na mitamba bora ya ng'ombe 620 ilinunuliwa na kusambazwa.

Madume bora ya mbuzi 80 na majogoo 1,400 yalisambazwa kwa wafugaji wa kata zote kumi  kupitia mradi wa PADEA.

Kwa upande wa kufufua vituo vya uhamilishaji kazi ilifanyika kwa kufufua vituo 9 katika kata za sita Machame Uroki,Machame Kaskazini,Machame Magharibi,Machame Mashariki,Masama Magharibi na Masama Mashariki.

Kwa upande wa viwanda,kuna kiwanda cha usindikaji wa maziwa cha Nronga na pia kuna vituo vya ukusanyaji wa maziwa kwa ajili ya kuuzwa katika mji wa Bomang’ombe pamoja na Moshi.Kadhalika wachinjaji 158 katika kata zote kumi walipatiwa elimu.

Ngozi vipande 176,000 vya ngozi za ng'ombe na mbuzi ziliandaliwa na kuuzwa na banda moja la ngozi limekarabatiwa.

Katika kuandaa nyama vizuri,wafanyabiashara 54 wa kata zote walipewa mafunzo juu ya ukataji nyama kwa kutumia misumeno ya umeme na misumeno ya kawaida.Aidha vikundi kumi vya wafugaji vya ushirika wa wafugaji viliundwa

Uvuvi

Kwa upande wa uvuvi,pamoja na kwamba wilaya yetu siyo maarufu kwa shughuli za uvuvi lakini uimarishaji wa uvuvi unafanyika na lengo la ilani lilikiwa kuzidisha mkazo katika kuzitumia maliasili zilizomo katika maziwa,mito na mabwawa ili wavuvi watumie fursa zilizopo kuinua hali ya maisha yao.

Mkakati ulikuwa ,moja kuwasaidia wavuvi kutumia maarifa ya kisasa ya uvuvi ili kuongeza ufanisi na mapato lakini mbili serikali za vijiji na mitaa kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kupambana na uvuvi haramu na tatu kuweka msukumo  maalumu katika ufugaji wa samaki katika mabwawa.Nne kuendeleza programu mahususi ya kuzalisha mbegu bora za samaki

Katika sekta hii ya uvuvi, elimu ilitolewa juu ya kupambana na uvuvi haramu katika vijiji vitatu vya Nronga na Kyeeri vilivyoko Machame Magharibi na Foo katika Machame Kaskazini.

Kwa upande wa doria zaidi ya doria ishirini zimefanyika katika mto wa Marire kata ya Masama Mashariki,mto Kikafu Machame Magharibi na Machame Kusini,mto Namwi uliopo Masama Mashariki na Magharibi na mto Semira uliopo Machame Kaskazini.

Kwa upande wa msukumo katika ufugaji wa samaki katika mabwawa,jumla ya mabwawa kumi na mawili yalichimbwa na kupandikizwa mbegu katika kata tano za Machame Magharibi,Masama Magharibi,Masama Rundugai,Machame Kaskazini na Hai Mjini.

Aidha elimu ya ufugaji wa samaki imetolewa kwa wafugaji 28 katika kata hizo tano za Machame Magharibi,Masama Magharibi,Masama Rundugai,Machame Kaskazini na Hai Mjini.

Elimu ya ufugaji wa samaki pia imetolewa kwa vijiji viwili vya Wari kilichopo Machame Kaskazini na Ng'uni kilichopo Masama Magharibi pamoja na vijiji hivyo kusambaziwa mbegu za samaki

Wanyamapori na Misitu

Kwa upande wa sekta ya wanyamapori na misitu,ilani ya uchaguzi ilijielekeza katika kuzipa serikali za mitaa nguvu zaidi na kuwawezesha wananchi kumiliki na kunufaika na maliasili

Kadhalika ilisisitiza na kuhimiza miji ianzishe bustani za ufugaji wa wanyamapori yaani zoo kwa maonyesho lakini pia ilisisitiza  kuweka utaratibu shirikishi wa upandaji wa miti,uvunaji na udhibiti wa moto

Jumla ya vikundi 14 vilipata mafunzo ya masuala ya hifadhi maliasili katika kata ya Machame Kaskazini, Machame Kusini,Machame Magharibi na Machame Mashariki.

Kwa upande wa ufugaji wa nyuki,katika wilaya yetu wengi kama mnavyofahamu shughuli za ufugaji zinafanyika hasa upande wa milimani katika vijiji vinavyopakana na msitu wa hifadhi wa mlima Kilimanjaro.

Kuna jumla ya vikundi 13 vinavyojishughulisha na shughuli za ufugaji wa nyuki,kuna mizinga 13,200 na kati ya hiyo mizinga 1,494 ni ya asili na mizinga 1,706 ni ya kisasa.

Kadhalika uzalishaji wa mazao ya nyuki katika wilaya umeweza kuongezeka kutoka wastani wa kilo 4,500 za asali kwa mwaka 2007/2008 hadi kufikia kilo 4,900 kwa mwaka 2010 na kwa upande wa nta kutoka kilo 150 mwaka 2007 hadi kilo 192 kwa mwaka 2010.

Kwa kifupi katika ufugaji wa nyuki kumekuwepo na mafaniko yakiwemo ya ongezeko la asali bora kutoka wastani wa tani 2 hadi kufikia tani 5 kwa mwaka,ongezeko la nta safi kutoka wastani wa kilo 50 hadi kilo 125 kwa mwaka,kupungua kwa matukio ya moto msituni mlima kilimanjaro kutoka matukio kumi mpaka kufikia manne,ongezeko la vikundi toka 7 mwaka 2005 hadi 13 mwaka 2010,ongezeko la mizinga ya kisasa toka 300 hadi 1,400,ongezeko la vifaa vya kurina asali kutoka seti 15 hadi seti 50 na ongezeko la mafunzo kwa wafugaji nyuki kwa mwaka 2007/2008 jumla ya wafugaji 4 walipata mafunzo na hadi kufikia mwaka 2010 jumla ya wafugaji 35 wameshapata mafunzo.

Kwa upande wa upandaji miti jumla ya miche 3,240,312 imezalishwa na katika kutoa mafunzo kwa wananchi wanaomiliki vitalu vya vya miche ya vijiji,jumla ya wamiliki 58 walipewa mafunzo katika kata zote za wilaya ya Hai.

Ushirika

Katika sekta ya ushirika.Ilani  ilisisitiza kuwa jukumu kubwa la sekta hii ni kuendeleza na kuimarisha ushirika wilayani.Malengo makuu ni kuimarisha ukaguzi wa vyama vya ushirika,kusimamia,kutoa na kuratibu mafunzo ya ushirika kwa wanachama,halmashauri na watendaji wakuu wa vyama vya ushirika ili kuboresha ushirika pamoja na kuhamasisha wananchi na vikundi vyenye shughuli za kiuchumi ili waunde vyama vya ushirika na vile vya akiba na mikopo yaani saccos.

Wananchi wa wilaya ya Hai wameendelea kuhamasishwa kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali ili kuondokana na umasikini.

Utelelezaji katika sekta ya ushirika hadi kufikia mwaka 2010 ni pamoja na wanachama waliongezeka kutoka 25,024 hadi kufikia wanachama 27,883,vyama vya ushirika wa akiba na mikopo navyo viliongezeka kutoka 20 hadi 30

Aidha  kumeweza kuwa na vyama vya ununuzi wa mazao hususani kahawa 25,vyama vya ushirika wa maziwa 7,vyama vya ushirika wa umwagiliaji maji 2,vyama vya ushirika vya uzalishaji biashara 2 na vyama vya ushirika vya uzalishaji asali kimoja.

Vyama vingi vya akiba na mikopo vijiji vilianza kutumia teknolojia ya kompyuta  katika kutunza mahesabu ya fedha za wanachama na vyama vya ushirika wa kuweka na kukopa yaani Saccos mbili zilianza mpango wa stakabadhi ghalani kwa mazao ya nafaka.

Vyama vya ushirika wa kuweka na kukopa yaani Saccos zenye mfumo huo zinawakopesha wanachama ili kuondokana na matatizo ya kijamii wakati wa kuuza mazao yao.

Aidha wanachama waliogeza hisa na kufikia shilingi 366,566,939,wanachama waliongeza akiba zao na kufikia shilingi 1,145,011,320,wanachama waliongeza amana na kufiki shilingi 385,659,298 na mikopo iliyotolewa kwa wanachama ilifikia shilingi 3,711,037,374.

2. SEKTA YA MIUNDOMBINU NA HUDUMA ZA KIUCHUMI

Hapa nitapitia katika sekta za ardhi,hifadhi ya mazingira pamoja barabara.

Ardhi

Katika ardhi,ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005 hadi 2012 iliweka mkakati wa kuendeleza kwa nguvu mpya kazi inayofanywa na halmashauri za wilaya katika katambua mipaka ya vijiji,kupima na kuvipatia vijiji hati za kumiliki ardhi.

Mbili kuendeleza kurahisha taratibu za upatikanaji wa hatimiliki za ardhi na tatu kuendelea kupima na kutayarisha ramani za msingi za nchi yetu kwa ajili ya kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo ya viwanja.

Katika eneo hili la ardhi mafunzo yalitolewa kwa vijiji 55. Kamati za ardhi zimeundwa katika kata zote,hati miliki zimeweza kuandaliwa na ramani zimetayarishwa.

Huduma za upimaji wa viwanja zilifanyika katika mji wa Hai,mashamba na mipaka ya ardhi katika maeneo mbalimbali ya vijiji ambapo jumla ya viwanja 7,045 vilipimwa na mashamba kumi na nne nayo yalipimwa.

Kwa upande wa vijiji,jumla ya vijiji 53 vilipimwa mipaka yake na vijiji viwili vya Uduru na Nshara havikukamilisha mchakato wake kutokana na mgogoro wa mpaka.

Barabara

Kwa upande wa barabara mkakati ulikuwa kuimarisha barabara na madaraja ya wilaya.

Wilaya ya Hai ina barabara zenye urefu wa kilometa 466.2 ,kati ya hizo kilometa 32 ni barabara kuu,kilometa 42 ni za mkoa,kilometa 175.93 ni za wilaya na kilometa 150.27 ni za vijiji.

Aidha katika ilani hiyo ya uchaguzi wilaya ya Hai ilipata bahati ya ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa lami kwa barabara ya Kwasadala hadi Masama yenye urefu wa Kilometa 12,

Katika mafanikio ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi kiasi cha kilometa 235.53 sawa na aslimia 50.82 za barabara zinapitika wakati wote.

Matengenezo ya kawaida ya barabara yalifanywa katika kata zote kwa kilometa 87.58 kila mwaka,matengenezo ya sehemu korofi kilometa 69 kwa kila mwaka na matengenezo ya muda maalumu kilometa 7.5 kwa kila mwaka.

Aidha barabara za kilometa 16.8 zilifanyiwa matengenezo ya muda maalumu katika kata zote kwa kila mwaka na madaraja na makalvati 126 yalitengenezea katika wilaya ya Hai.

Kwa upande wa barabara ya Kwasadala hadi Masama mpaka sasa kiasi cha kilometa nne kimeshawekwa tabaka la awali la lami.

Lakini pia mheshimiwa rais katika ziara yake ya mwaka jana aliahidi kuongeza zaidi barabara hiyo kwa kilometa nne ili iweze kuungana na barabara ya Machame kutoka masama ambayo nayo ni ya lami pamoja na kuongezaia kipande kingine ambacho kitainganisha na barabara inayoelekea wilayani Siha ambayo nayo ni ya lami.

Hifadhi ya mazingira

Ilani ya uchaguzi iligusa eneo la maliasili na mazingira kwa kuelekeza kuongeza kasi ya utekelezaji wa sera ya taifa ya mazingira ya mwaka 1997 na sheria ya usimamizi wa mazingira ya mwaka 2004.

Mikakati ya hifadhi ya mazingira katika ilani ilikuwa ni pamoja na moja kukabiliana na uharibifu wa mazingira na kutoa elimu kwa wananchi ili kuongeza uelewa wao kuhusu hifadhi ya mazingira.Lakini pili kujenga mwamko katika jamii wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchini.

Tatu kuendeleza kampeni ya upandaji wa miti ambayo imekuwa ikifanywa kila mwaka na kuhakikisha kwamba miti inayopandwa inatunzwa ipasavyo na kuhimiza sheria ya kutokata miti

Nne kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kutenganisha taka ngumu ili  kudhibiti uchafuzi wa mazingira

Na tano kuhamasisha sekta binafsi kuanzisha viwanda vitakavyotumia taka ngumu malighafi.

Wilaya ya Hai ina eneo la misitu la hekta 14,154 ambazo ni sawa na asilimia 14 ya eneo lote la wilaya na kutokana na msongamano mkubwa wa makazi ya watu,ongezeko la watu,mashamba na mifugo inasababisha wilaya kuwa na matukio ya uharibifu wa mazingira.

Katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wilaya iliweza kuweka mikakati mbalimbali ikiwemo ya kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kuhifadhi,kulinda na kutunza mazingira kupitia redio.

Aidha vipeperushi 34,000,mabango 3,600 na vijarida 18 vilisambazwa na pia elimu ya hifadhi ya mazingira imetolewa katika kata kumi.Jumla ya miche ya miti 19,408,311 imeoteshwa na kutunzwa katika kipindi hicho cha miaka mitano.

Aidha kulikuwa na warsha  zaidi ya tano na zilizowahusisha  wadau 650 wa mazingira katika mji wa Bomang'ombe. Pia elimu kwa njia ya radio ilitolewa.Elimu na sheria ya mazingira imetolewa katika vijiji vyote .

3. SEKTA YA HUDUMA ZA JAMII
Katika eneo hili la Ilani tutaingia zaidi katika elimu,afya na maji

 Sekta ya elimu

Tuanze na elimu ya awali ambapo mkakati ulibainisha kuongeza kasi ya upanuzi kwa kuhamasisha sekta binafsi na kuhakikisha kuwa sera ya kila shule ya msingi kuwa na darasa la awali inatekelezwa

Katika utekelezaji wa ahadi hiyo wilaya  ina jumla ya   madarasa 116 ambapo 101 ni ya serikali na 15 ya binafsi yenye uwezo wa kuchukuwa watoto 4,401.

Elimu ya msingi

Kwa upande wa shule ya msingi ahadi ilikuwa kuandikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule na kufikia asilimia 100 ifikapo mwaka 2010.

Lakini pia kuongeza uandikishaji wa watoto wenye ulemavu na wengine wenye matatizo maalumu na pia kujenga na kupanua miundombinu ikiwa ni pamoja na nyumba za walimu,madarasa,vyoo na huduma zinazohusika.

Lakini pia ilani ilisisitiza kuendeleza kuhakikisha kwamba maslahi ya walimu yanaboreshwa na kulipwa kwa wakati.

Kuendelea kuimarisha ukaguzi wa shule ili kuimarisha ubora wa elimu na kuongeza asilimia ya wanafunzi kujiunga na sekondari kufikia asilimia hamsini ifikapo 2010.

Wilaya ya Hai ina jumla ya shule za msingi 119 ambapo kati ya hizo 104 ni za serikali na 15 za binafsi.

Kwa upande wa shule ya msingi malengo ya ilani yalifanikiwa kwa watoto wote wenye umri wa kwenda shule kuandikishwa kwa asilimia 95

Kwa upande wa ufaulu,kiwango kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka mfano ,mwaka 2007 wilaya ilifaulisha kwa asilimia 48.73,mwaka 2008 kwa asilimia 55.84,mwaka 2009 kwa asilimia 62.8 na mwaka 2010 kwa asilimia 74.5.

Kwa upande wa watoto wenye ulemavu,madarasa zaidi yalijengwa katika shule maalumu ya walemavu ya St.Francis na kuweza kuandikisha watoto kutoka  katika kata za Hai mjini na masama mashariki

Aidha katika kipindi hicho jumla ya vyumba vya madarasa 32 yalijengwa na kufanya wilaya kuwa na jumla ya vyumba 780,nyumba za walimu 15 na kufanya wilaya kuwa na nyumba za walimu 129.

Jumla ya matundu  112 ya vyoo yalijengwa na kufanya wilaya kuwa ma matundu ya vyoo 1321

Madawati 762 yalitengenezea katika kata zote kumi na jumla ya walimu 111 waliokuwa wanadai maslahi yao na kustahili kulipwa walilipwa na walimu 555 walikwenda masomoni.

Elimu ya sekondari

Kwa upande wa elimu ya sekondari mpango ulikuwa kisimamia kwa ukamilifu utekelezaji mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari yaani MMES,pia kuongeza idadi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka cha nne na kufikia asilimia hamsini ya watoto wa rika lengwa la umri wa miaka kumi na nne mpaka kumi na saba ifikapo mwaka 2010

Wilaya ya Hai inazo jumla ya shule za sekondari 44 ambazo 29 ni za serikali na 15 ni za binafsi.

Katika sekondari jumla ya vyumba vya madarasa 183 vya sekondari vimejengwa katika kata zote  na kufanya wilaya kuwa na jumla ya madarasa 294.

Kadhalika kuna maabara 14,jumla ya nyumba za walimu 24 zilijengwa na kufanya wilaya kuwa na nyumba 82 na maktaba mbili.

Aidha kiwango cha ufaulu kilifikia wastani wa asilimia 53.1 kwa kidato cha nne

Kwa upande wa sekondari za kidato cha tano na sita wilaya ilikuwa na shule mbili tu ambazo sekondari ya Lyamungo na sekondari ya Machame hivyo wilaya  imeendelea na upanuzi wa shule za sekondari za serikali ili ziwe na nafasi za kidato cha tano na sita.shule hizo ni Hai Day,Lemira,Nkokashu,Lyasika na Harambe.
Elimu ya watu wazima

Kwa upande wa elimu ya watu wazima ilani ililenga kufufua mpango wa awali wa elimu ya watu wazima na kuendelea kuboresha elimu ya watu wazima kwa kutumia mbinu shirikishi ya walengwa watakaojifunza  kuandika,kuhesabu na kusoma na hivyo kuwasaidia  kuongeza ujuzi katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii.

Na mwisho kuimarisha mpango wa elimu ya msingi kwa walioikosa yaani MEMKWA.

Katika elimu ya watu wazima jumla ya vikundi 119 vilianzishwa kwa kata zote na watoto walitambuliwa na kupelekwa shule za Machame Mashariki wakiwa  70.Hai Mjini 66,Masama Rundugai  34.Aidha jumla ya madarasa ya MEMKWA sita yalifunguliwa.


 Sekta ya afya
Ilani ilitilia mkazo kuendelea uboreshaji wa huduma za afya.

Mikakati ilikuwa ni pamoja na kuongeza jitihada za kupambana na magonjwa ya milipuko kama  kipindupindu yanayojitokeza mara kwa mara.

Kupambana na magonjwa yanayoongoza ambapo katika wilaya ya Hai ambayo ni pamoja na Malaria,magonjwa ya uambukizo wa njia ya hewa,magonjwa ya kuhara,minyoo,nimonia,magonjwa ya macho,magonjwa ya kinywa na meno,magonjwa ya masikio na magonjwa ya ngozi.Lakini kati ya magonjwa hayo yanayoongoza kwa vifo ni malaria na nimonia.

Kupunguza vifo vya watoto wachanga kutoka 95 kwa kila vizazi 1000 hadi kufikia vifo 50 kwa kila vizazi 1000,

Kupunguza vifo vya watoto chini ya umri wa miaka mitano kutoka vifo 154 kwa kila watoto 1000 wanaozaliwa hadi vifo 79 kwa kila watoto 1000 wanaozaliwa.

Kupunguza vifo vya uzazi kutoka 529 kati ya wazazi 100,000 kwa sasa hadi kufikia 265 kwa wazazi 100,000 kwa mwaka.

Ahadi ya ilani pia iliweka msisitizo wa kuongeza kiwango cha wazazi wanaojifunguza kwa wakunga wanaopata mafunzo kutoka asilimia 50 hadi kufikia asilimia 80 mwaka 2010.

Kadhalika kuzipatia vifaa vya kisasa hospitali,vituo vya afya na zahanati za serikali.Ujenzi na ukarabati wa majengo ya kutolea huduma

Katika mafanikio yaliyopatika,wilaya ina jumla ya hospitali mbili,hospitali ya wilaya na hospitali teule ya wilaya,yaani hospitali ya Machame inayomilikiwa na kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania,KKKT dayosisi ya kaskazini.

Aidha kuna vituo vya afya sita katika vituo hivyo vinne vinamilikiwa na serikali na viwili vina milikiwa na mashirika ya dini na watu binafsi.

Zipo jumla ya zahanati hamsini na moja ambapo ishirini na sita ni za serikali,kumi zinamilikiwa na mashirika ya dini na kumi na tano za watu binafsi.

Jumla  ya vyoo bora 1,216 vimejengwa na watumishi 87 walipatiwa mafunzo rejea katika vituo vya afya 40 vilivyoko wilayani kwa ajili kupambana na magonjwa ya mlipuko.

Katika kupunguza vifo vya watoto wachanga mafunzo ya muda mrefu na mfupi yametolewa kwa watumishi pamoja na chanjo za kinga zimetolewa kwa wajawazito wote kwa asilimia mia moja katika vituo vyote 40 wilayani.

Hutoaji wa chanjo umeongezeka ambapo chanjo ya BCG imefikia kutolewa kwa asilimia 95,Surua asilimia 92,DPT HB HIB asilimia 92 na polio asilimia 92.

Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana hutoaji wa chanzo umefikia asilimia 97 kwa magonjwa ya pepopunda,polio,kifua kikuu,kifaduro,dondakoo,homa ya ini,homa ya uti wa mgongo na kichomi.

Katika kupunguza vifo vya watoto chini ya umri wa miaka mitano,masomo ya ndani yalitolewa kila mwezi mara moja kwenye hospitali ya wilaya kwa watumishi 25

Kadhalika wilaya ina majokofu ya umeme au gesi kwa ajili ya kuhifadhi dawa za chanjo katika ubaridi unaotakiwa kwa  vituo vyote 40.

Hadi kufikia mwaka 2013 wilaya imeweza kuongeza huduma kwa kufikisha vituo vya huduma 47 na kliniki za masafa na mikopba 16.

Wajawazito wote wanaohudumiwa kliniki wanapatiwa punguzo kwa ajili ya vyandarua.Akinamama wajawazito 4895 walipatiwa vyandarua kwa mwaka 2010,

Katika kupunguza vifo vya uzazi mafunzo rejea yametolewa kwa wakunga 25 na gari moja la kubebea wagonjwa limenunuliwa na kukabidhiwa kwa hospitali ya wilaya.

Katika kuongeza idadi ya wazazi wanaojifunguz kwa  wakunga,mafunzo ya rejea yametolewa kwa wakunga na vifaa vya afya vimesambazwa kwenye zahanati 23 na vituo vyote 4 wilayani.

Kiwango cha akinamama wanaojifungulia katika vituo vya huduma za afya kimeongezeka kutoka asilimia 47 kwa mwaka 2008 hadi kufikia asilimia 62 mwaka 2010.

Akinamama waliopata kinga dhidi ya malaria ni sawa na asilimia 68 na waliopata chanjo ya pili ya pepopunda ni asilimia 90.7

Jumla ya vituo vya afya 14 vilifanyiwa ukarabati.Nyumba 12 za watumishi zimefanyanyiwa ukarabati.

Katika kupambana na ugonjwa wa malaria utoaji wa tiba sahihi kwa wagonjwa umeendelea kutolewa kwa kutumia dawa mseto,kutoa mafunzo kwa wataalamu wa afya na kutoa elimu kwa jamii juu ya utambuzi wa dalili za awali za malaria na hatua inayopaswa ichukuliwe.

Ukimwi
Ilani imeelekeza kuimarisha vita dhidi ya ukimwi.

Mikakati ilielekeza kuimarisha vita dhidi ya ukimwi ikiwa ni pamoja na kutumia vizuri misaada ya wahisani na kuelimisha wananchi dhidi ya unyanyapaa.

Kufikisha elimu kuhusu ugonjwa wa ukimwi kwa wananchi mitaani na vijijini na kuimarisha mpango wa kutoa dawa za kurefusha maisha na kupunguza makali kwa wanaoishi na virusi vya ukimwi.

Katika utekelezaji wa mapambano dhidi ya ukimwi vituo 44 vya kupimia virusi vya ukimwi vimeongezeka,jumla ya vituo vya ushauri nasaha 52 vimeongezeka na jumla ya kamati 48 zimeongezewa uwezo kwa kupatiwa magunzo.

Wahudumu 42 wa majumbani na asasi 39 zilishirikishwa katika hutoaji wa dawa katika hospitali ya wilaya.

Vituo 39 vya afya na kliniki nne vinatoa huduma na jumla ya watu 96,265 walipimwa virui vya ukimwi.

Katika mwaka 2010 kufuatia mheshimiwa Rais kuzindua kampeni ya watu kupima virusi kwa hiari jumla ya watu 27,247 walijitokeza kupima ambapo watu 611 sawa na asilimia 2.2 walipatikana na maambukizi ya Virusi vya ukimwi.

Maji
Kwa upande wa maji ilani iliweka mkazo katika kuendelea kutekeleza sera ya taifa ya maji ya mwaka 2002.

Mkakati wa ahadi hiyo ni pamoja na kuwawezesha wananchi mjini na vijijini kupata maji safi,salama na ya kutosha kwa matumizi yao ya kawaida karibu na sehemu wanazoishi na mahitaji ya kiuchumi kwa kufanikisha hiduma hiyo kwa asilimia 90 ya wakazi wa mjini na asilimia 65 ya wakazi vijijini ifikapo 2010.

Kushirikiana na wananchi katika hatua ya kutoa huduma ya maji kwa kupanga kujenga,kuendesha na kumiliki miradi ya maji mijini na vijijini sambamba na kuimarisha mifuko ya maji ambayo imeanzishwa na wananchi.

Kuhimiza,kuimarisha na kupanua teknolojia nyepesi na rahisi na kukinga,kutunza na kutumia maji ya mvua.

Katika utekelezaji wa ilani kuhusu maji wilaya ya hai inapata huduma ya maji kupitia skimu sita za mtiririko ambazo ni Uroki Bomang'ombe,Losaa Kia,Lyamungo Umbwe,Maili sita,Machame na Mkalama.

Jumla ya vijiji hamsini na mbili vinapata maji safi na salama katika umbali wa mita 400 ambapo ni sawa na asilimia 82 ingawa kwa viwango tofauti.Vijiji ambavyo havina huduma ya maji safi na salama ni Mbatakero,Ngosero na Mtakuja.

Aidha  miradi mipya ya maji ilifanyiwa usanifu katika kata za masama rundugai,machame kusini,masama mashariki na masama magharibi.

Wilaya ya hai ina miradi katika vijiji 13 katika kata za machame kusini pamoja na masama rundugai.

Aidha kamati za maji 29 katika kata za masama rundugai,machame kusini,machame mashariki na machame kaskazini ziliundwa.

Mifuko ya maji 16 iliundwa ili kusimamia na kuendesha miradi ya maji kupitia bodi za wadhamini.Bodi hizo zimeundwa na jamii na kusajiliwa kisheria kama inavyotakiwa na sheria ya maji na usafi wa mazingira namba 12 ya mwaka 2009

Teknolojia ya uvunaji wa maji ya mvua inaendelezwa hasa katika ukanda wa  tambarare.Matenki 36 ya kuvuna maji ya mvua yamejengwa katika taasisi mbalimbali za serikali hususani shule za msingi ambazo ni pamoja na shule za Kikavu chini,Nguzone,Ngosero Mbatakero,Mkalama,Kawaya, Chekereni,Uhuru,Weruweru, Mijongweni,Mgungani,Maili sita,Shirinjoro,Tindigani,Mtakuja SanyaStation,Usari,Narumu Tela,Mulama,Narumu, Usari,Kilanya,Sere, Nkweseko, Machame,Nshara na Nkwamwasi.

kadhalika matenki hayo yamejengwa katika sekondari ya Longoi na zahanati  za Bomang'ombe,Sanya station,Ngosero,Mkalama pamoja na ofisi za makao makuu ya wilays,idara ya maji na soko la walaji la mjini hai.

4. UTAWALA BORA

Katika utawala bora ilani ilijikita zaidi katika kuendelea kuimarisha utawala bora kwa kuhakikisha kwamba nchi inaendeshwa kwa misingi ya sheria,kanuni na taratibu zilizowelwa za kidemokrasia

Mkakati uliwekwa ni pamoja na kutoa mafunzo juu ya utawala bora kwa watendaji  katika ngazi zote na kuhakikisha kwamba matokeo ya mafunzo hayo yanaiweka serikali kwenye utendaji ulioko wazi.

Katika utekelezaji mafunzo yalitolewa kwa maofisa watendaji wa vijiji vyote ,maofisa watendaji  wa kata zote 10,wenyeviti wa vitongoji 249 na mtaa 11.

5. DEMOKRASIA NA MADARAKA YA UMMA
Ilani ililenga katika kujenga mfumo wa demokrasia imara wenye kuheshimu haki ya wananchi katika ngazi zote.

Mikakati ulielekezwa zaidi katika kujenga utamaduni unaoheshimu haki ya wananchi wa kujadili na kuhoji mambo yanayohusu nchi yao na kuheshimu dhamana na haki ya vyombo halali vya kutekeleza maamuzi yaliyofikiwa kihalali ili shughuli za nchi ziendelee

Kadhalika kuhakikisha utaratibu wa wananchi kuchagua viongozi wao kwa misingi ya demokrasia unadumishwa.

Kushirikisha wananchi katika kupanga na kusimamia maendeleo yao.kuhimiza serikali za mitaa ziunge mkono juhudi za wananchi za kupambana na umasikini.

Na pia kuhakikisha serikali za mitaa zinakua na mipango mizuri itakayoziongezea mapato yatakayosaidia kutoa huduma bora za jamii.

Katika eneo hili la demokrasia jumla vikao vya ngazi mbalimbali vya kisheria vilifanyika vikiwemo vya kamati ya maendeleo ya kata vikao 40,serikali za vijiji 260 na vitongoji 490.

Chaguzi za viongozi wa serikali za mitaa zilisimamiwa na tamisemi na kufuata kanuni na taratibu za sheria za uchaguzi oktoba 2009

Mwaka 2007 nafasi ya udiwani wa kata ya masama kusini ilijazwa baada ya aliyekuwa diwani kufariki dunia.pia vitongoji viwili vya marukeni na mbosho vilijaza nafasi za uongozi mwaka 2009.

Mipango ya maendeleo vijiji iliibuliwa katika kata zote kumi na vijiji vyote 55 na vitongoji 11.Elimu ya kuiwezesha jamii kujitegemea na kujenga uwezo wa kubaini firsa ma vikwazo vya maendeleo yaani O & OD imetolewa kwa kata zote kumi na wananchi wanaibua miradi shirikishi kwa kuzingatia vigezo vya vya fursa na vikwazo vya maendeleo yaani o& od.

Jumla ya shilingi milioni 76.5 zilichangwa kwenye miradi ya wananchi kutokana na asilimia tano ya mapato ya halmashauri

Vyanzo vipya vya mapato vilibuniwa kila mwaka.Pia tunaendelea kuboresha vyanzo vilivyopo.Halmashauri ina uwezo wa kujitegemea kwa asilimia 20 tu.

6. UTAMADUNI NA MICHEZO
Utamaduni

Katika utamaduni na michezo  ilani imeelekeza kwamba mkakati ulikuwa kuenzi na kulinda historia,mila na desturi nzuri za wananchi wetu na kuzitokomeza mila na desturi mbaya.

Imetaka jamii ihamasishwe kuthamini na kutunza tamaduni zao kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Lakin pia kuhimiza matumizi ya sanaa katika kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya jamii

Katika utekeleza wa eneo hilo semina nne zilizotolea katika kata za masama rundugai na hai mjini na pia kamati za utamaduni za kata ziliundwa kwenye kata za machame kaskazini,masama mashariki na masama rundugai.

Sheria ndogo ya kuhifadhi Maeneo ya utamaduni wa kihistoria na vivutio vya utalii vilivyopo hai imetungwa kwa lengo ya kuhakikisha maeneo hayo yamehifadhiwa kama vile chemchem ya maji moto ya chemka katika kata ya masama rundugai,maporomoko ya maji yaliyopo Nshara na kijiji cha utamaduni wa maasai kilichopo Sanya Station.

Vikundi vya sanaa vilianzishwa ambapo jamii imehamasika kuunda vikundi vya utamaduni na mpaka sasa vikundi zaidi ya tisa tayari vimeshaundwa na vimefaniwa kutengeneza katiba zao na vikundi hivyo vinajiendesha vyenyewe kwa baadhi kutoa burudani nyakati za sherehe katika kata za machame kusini,hai mjini,machame uroki,masama mashariki na masama rundugai.

Kadhalika wilaya imeweza kutengeneza mazingira ya wanafunzi wenye vipaji katika sanaa na utamaduni kuvionyesha hususani uchoraji,uigizaji,ususi,ufinyanzi na uimbaji kupitia mpango uliowekwa wa kuhamasisha wanafuni kuonyesha vipaji vyao.

 Michezo

Katika eneo la michezo,ilani imeelekeza   Utekelezaji wa sera ya taifa ya michezo ya mwaka 1995.

Mkakati uliowekwa ni pamoja na kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli za michezo na kuhamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za michezo

Wilaya ilijiwekea malengo ya kuhakikisha jamii ina hamasika kushiriki kikamilifu katika michezo yote ikiwemo michezo ya kitaalamu na michezo ya jadi.

Katika utekelezaji maeneo ya michezo yaliyotengwa na kulindwa katika shule zote na klabu 10 za mpira wa miguu zimeundwa katika kata zote kumi na pia taasisi za kiserikali ikiwemo halmashauri ya wilaya,polisi wilaya na veterani zimeunda timu kwa kila mchezo katika timu za mpira wa miguu,wavu,mikono na riadha.

Timu za wanafunzi za shule za msingi na sekondari zimeshiriki kikamilifu katika michezo ya kitaifa ya umitashumta na umiseta.

Vyama mbalimbali vya michezo vimeanzishwa kama chama cha mpira wa miguu cha wilaya,chama cha mpira wa wavu cha wilaya na chama cha riadha cha wilaya na chama cha mchezo wa jadi na bao.

Viwanja vimetengwa vya michezo katika kata zote.

7.KUENDELEZA MAKUNDI MBALIMBALI
Ilani pia iligusa makundi mbalimbali ambayo ni pamoja na watoto,wanawake na vijana


Watoto

Tukianza na  watoto,ilani ililenga kuimarisha utaratibu wa mashirika ya hiari na watu mbalimbali wanaoshughulikia vituo vya kulea watoto pamoja na shule za awali

Katika utekelezaji jumla ya vituo vinne vya kulelea watoto yatima vilianzishwa katika kata za hai mjini.masama kusini na machame kusini

Aidha mashirika ya dini na yasiyo ya kiserikali yalianzisha vituo vya kulelea watoto katika kata zote  za wilaya ya hai.

Wilaya imeweza kuunda kamati za kutambua na kusimamia huduma za watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi kwa vijiji vyote.

Mpango huo ulipunguza uwezekano wa mtoto mmoja kupata huduma kutoka kwa zaidi ya wadau mmoja wakati wapo watoto wanaokosa kabisa.

Wilaya inao watoto 68,229 kati ya hao 5,088 wanaishi katika mazingira hatarishi waliweza kutambuliwa na kuanza kupewa huduma vijijini mwao,halmashauri na wadau mbalimbali.

Huduma wanazopewa ni pamoja na ada za shule watoto 3,202,huduma za afya watoto 3,153 na malazi kwa watoto 200.

Wanawake

Kwa upande wa wanawake ilani imeeleza kuwa lengo ni kuendelea kutekeleza sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia

Na mikakati iliyoanishwa ni pamoja na kuongeza nafasi ya viti maalumu katika chaguzi za mitaa,vitongoji,kamati za shule,kamati za maji,kamati za zahanati,kamati mbalimbali za bunge za taifa na ubunge na uwakilishi.

Kadhalika kuimarisha mifuko ya mikopo mbalimbali ya wanawake ili waweze kufaidika zaidi.

Katika utekelezaji jamii imeendelea kuelimishwa itambue uwezo wa wanawake na umuhimu wa kupewa fursa ya elimu na ajira katika kata za masama mashariki,machame kaskazini na masama rundugai.

Wilaya imeweza kuwahamasisha akina mama kuunda vikundi vya ujasiriamali ili kuondokana na umasikini ambapo wameweza kuanzisha vikundi 250 na kujihusisha na kilimo,ufugaji wa ng'ombe wa maziwa,mbuzi wa maziwa,kuku,biashara ya mazao sokoni,upambaji na mapishi.

Aidha halmashauri ya wilaya ilitoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni kumi na sita kutoka mfuko wa maendeleo ya wanawake kwa vikundi tisa kwa dhumuni la kuwawezesha kukuza mitaji yao.

Vikundi hivyo vimepatiwa mafunzo ya itunzaji wa kumbukumbu za miradi na itaratibu wa urejeshaji wa mikopo hiyo

Vijana

Kwa upande wa vijana ilani imeeleza lengo ni kutekeleza sera ya taifa ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996.

Mikakati kwa upande wa vijana ililenga kuimarisha mfuko wa maendeleo ya vijana katika halmashauri ili uweze kuwanufaisha vijana wengi zaidi kwa usimamizi mzuri na kuwezesha mfuko huo kuwa endelevu.

Wilaya ya Hai ina vijana zaidi ya 169,847 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002.

Katika utekelezaji wake vikundi 18 vya kiuchumi vya vijana vilianzishwa na vilipata mikopo kipitia vyama vya mikopo vikiwemo BRAC, na USAWA,NMB,CRDB,SEDA,SACCOS na FAIDA.

Hitimisho

Huo ndio utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wa mwaka 2005 mpaka 2012 zikiwa ni ahadi ya serikali ya awamu ya nne katika kipindi chake cha awali cha miaka mitano baada ya kupata ridhaa ya wananchi na miaka miwili ya awamu ya pili ya 2010 hadi 2012.

Kwa mukhtasari pamoja na mafaniko makubwa katika utekelezaji wa ilani bado pana changamoto katika baadhi ya maeneo yakiwemo ya wilaya kukabiliwa na ukame wa mara kwa mara kutokana na mvua chache,uharibifu wa mazingira hususani ukataji wa miti,barabara nyingi bado za udongo na hivyo kuharibika kwa muda mfupi,upungufu mkubwa wa watumishi pamoja na wilaya kukosa  viwanda na kuwepo kwa tatizo la ajira hasa kwa vijana.

Kutokana na changamoto hizo wilaya imejipanga katika kuongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji maji kutoka hekta 17,030 za sasa na kufikia hekta 18,530 ifikapo mwaka 2015,wilaya ina mkakati wa kujenga zahanati kwa kila kijiji ili kusogezs huduma za afya kwa wananchi,wilaya inakuimarisha zao la kahawa na ufugaji bora wa ng'ombe wa maziwa ili yawe mazao makuu ya biashara kwa wananchi,kuziimarisha barabara za wilaya na vijiji,mkakati wa kujenga masoko ya mazao ya wakulima katika maeneo ya masama mula na lyamungo,kukamilisha shule tano za kidato cha tano na sita na kutekeleza programu ya kitaifa ya maji vijijini katika vijiji vyote tisa vilivyoibua miradi ya maji.

Asanteni kwa kunisikiliza


Novatus Makunga,Mkuu wa wilaya ya Hai

 


186 YOUTH TO JOIN SECURITY TRAINING PLAN IN HAI

Posted by MK On 09:03 No comments



Monday, 21 January 2013 09:12

By The Citizen Reporter,Bomang'ombe



At least 186 young people in Machame East Ward, Hai District, Kilimanjaro Region, have volunteered to undergo paramilitary training offered by the People’s Militia to enhance security in the area, it was announced at the weekend. Upon graduation, 85 of them would be hired to increase security on the slopes of Mt Kilimanjaro and check illegal loggers and invaders of water sources. 


Others would be deployed to check illegal brewing and sale of liquor, bush fires and indiscriminate felling of trees, according to district commissioner Novatus Makunga. 


Speaking during the closing of another training programme at Mroma Village, he said a special training programme for 186 candidates, who had registered for the People’s Militia programme would start soon. 


The DC urged Hai residents to disregard the propaganda spread by some people, who were opposed to People’s Militia concept, some associating it with the ruling Chama cha Mapinduzi (CCM) and others saying undergoing such a training programme was a wastage of time and resources. 


He told them that the People’s Militia unit was part of a reserve army because it complemented security and defence organs in fighting against crime, especially in rural areas and densely populated suburbs.


Mr Makunga, who is the chairman of the defence and security committee in the district, said the Police Force could not manage to provide security by 100 per cent in all districts and regions and, therefore, the People’s Militia had to help in that regard. 


The People’s Militia programme, he explained, was pioneered by the Father of the Nation, Mwalimu Nyerere, who declared in the 1960s that the defence and security of Tanzania lied solely in the hands of Tanzanians themselves. The People’s Militia was created by the Reserve Forces Act, 1965 to serve as a national reserve and ensure that the TPDF had the monopoly of military power in the country. 


Mr Makunga ordered that private security firms should give priority in recruitment and hiring to security guards who had gone through the People’s Militia training programme because it was easy to verify their capability and past records.



For his part, Hai District Council chairman Clement Kwayu told residents not to ignore the People’s Militia programme,saying it was part of the country’s public order organs.



SOURCE: http://www.thecitizen.co.tz/news/4-national-news/28279-186-youth-to-join-security-training-plan.html